Jumatano, 10 Agosti 2016

Mawakala wa bia wa TBL wajishindia Pikipiki za usambazaji

Postedy by Esta Malibiche on August 10.2016 in BIASHARA

MA1
Mkurugenzi wa kamapuni ya Kibogoyo ya jijini Dar es Salaam, inayojihusisha na usambazaji wa vinywaji vya TBL,Jackson Mtei (katikati) akijaribu kuwasha  pikipiki yake ya matairi matatu aina ya Toyo,  huku Mkurugenzi wa Mauzo na Usambazaji wa TBL Group  Gareth Jones (Kushoto) akimshangilia wakati alipoibuka mshindi kwa kuvuka malengo ya usambazaji wa vinywaji  vya kampuni hiyo.   kulia ni Meneja wa  Mauzo na Usamabazaji na TBL Group  Kanda ya Kusini ,James Bokella, wakati wa hafla iliyofanyia katika kituo cha mauzo cha Ubungo .
MA2
Mkurugenzi wa Mauzo na Usamabazaji wa TBL Group  Gareth Jones (Kushoto) akimkabidhi Mkurugenzi wa kampuni ya Rassam ya Banana Ukonga jijini Dar Es Salaam, Mwita Magaiwa   Ufunguo wa pikipiki  ya matairi Matatu  aina Toyo, mara baada ya kuibuka mshindi kwa kuvuka malengo ya usambazaji wa vinywaji  vya kampuni hiyo. Kulia ni Meneja wa  Mauzo na Usamabazaji na TBL Group  Kanda ya Kusini ,James Bokella. Hafla hiyo  iliyofanyia katika kituo cha mauzo cha Ubungo .
……………………………………………………………………………………………………
Mawakala watatu  wa  kampuni ya TBL  Group wanaofanyia biashara zao jijini Dar es Salaam wamejishindia pikipiki za  usambazaji aina ya Toyo  kila moja ikiwa na thamani ya shilingi milioni 3.9 baada ya kuibuka washindi katika kampeni ya mauzo ambayo ilikuwa inaendeshwa na kampuni kuanzia Mwezi Mei mwaka huu.
Hafla ya kukabidhi  pikipiki hizo za kubebea mizigo imefanyika katika kituo cha  mauzo cha TBL Group cha Ubungo jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na wateja na maofisa mbalimbali kutoka kampuni hiyo.
Akiongea wakati wa kukabidhi zawadi hizo,Mkuu wa kituo cha Mauzo na Usambazi wa TBL kanda ya Kusini,James Bokella,alisema kuwa kampeni hiyo iliyolenga kuwawezesha mawakala wadogo wa kampuni hiyo imefanyika kwa kipindi cha miezi mitatu na kuwashirikisha wafanyabiashara 117 ambapo miongoni mwao watatu wamevuka lengo la mauzo lililokuwa limewekwa na kampuni na wamefanikiwa kujishindia pikipiki za kubeba mizigo aina ya Toyo.
Aliwataka wafanyabiashara hao kuwa ni Rasam Traders wa Ukonga,Kupata Kuna Mungu Shop wa Mbagala na Kibongoto Investment wa Sinza “Wafanyabiashara hao wamefanya vizuri katika kipindi cha kampeni ya kuvuka lengo la mauzo ambalo  kampuni ilipanga na leo wanakabidhiwa pikipiki za kubebea mizigo kwa ajili ya kuwarahishia  shughuli zao za biashara hususani usambazaji wa vinywaji”.Alisema Bokella.
Aliongeza kuwa  kampeni hii ni mwendelezo wa promosheni za kampuni kupitia mpango wa kuwaendeleza wafanyabiashara wanaosambaza bidhaa zake na mbali na kuwapatia zawadi pia imekuwa na utaratibu wa kuwapatia mafunzo mbalimbali kwa ajili ya kukuza biashara zao ambapo wamekuwa wakipatiwa mafunzo ya ujasiriamali,utunzaji wa vitabu vya fedha,matumizi mazuri ya fedha zao,usafi katika maeneo yao ya biashara na kanuni na sharia za kufanya biashara nchini.
Alisema kampuni hiyo maarufu kama Retail Development Programme imepata mafanikio makubwa kwa kuwafikia wafanyabiashara wengi wanaosambaza bidhaa za kampuni na hivi sasa biashara zao zimeimarika zaidi na mitaji yao kuongezeka na kuwafanya waishi maisha bora pamoja na familia  zao.
Baadhi ya wafanyabiashara walioibuka washindi katika kampeni hii wameishukuru kampuni ya TBL Group kwa kubuni promosheni zenye mwelekeo wa kuboresha maisha ya wateja wake “Ninayo furaha kujishindia pikipiki ya kusambazia vijana,ushindi huu unadhihirisha kuwa tunafanya kazi na kampuni inayotujali wateja wake”.Alisema mmoja wa washindi Mwita Magaiwa anayemiliki biashara ya Rasam Traders.
Mshindi Mwingine Jackson Mushi mmiliki wa Kibongoto Investment amesema kuwa inatia moyo kuona wawekezaji wakubwa kama TBL wanabuni mikakati ya kukuza wafanyabiashara wadogo kama ambavyo wametoa pikipiki za kusambazia vinywaji “Zawadi hii zinazidi kutupa motisha ya kufanya kazi kwa bidi”.Alisema

0 maoni:

Chapisha Maoni