Jumatano, 17 Agosti 2016

ZIFAHAMU FAIDA ZA KULA BAMIA

Postedy by Esta Malibiche on August 17.2016
 
Chimbuko la Bamia ni Abyssinia (Ethiopia) Kisha ikaenea Duniani kote.
1. Michirizi na utonvu unaopatikana katika Bamia, husaidia kusawazisha Kisukari kwa kuzuia kiwango cha Sukari inayotumika katika mwili kutoka kwenye utumbo mkubwa.
2. Utelezi wa bamia huchuja uchafu unaoingia katika Kolestorali (cholesterol) na asidi ya Nyongo unaoingia kutoka kwenye Ini ambao usipo dhibitiwa huenda ikasababisha matatizo ya ki-afya.
3. Bamia husaidia kulainisha Utumbo mkubwa (large intestines) kutokana na kazi yake ya kulainisha choo.
4. Bamia hutumika kwa kutibu vidonda vya Tumbo inasaidia kusawazisha Asidi.
Magonjwa Maalum
Asidi ya Kujirudia rudia na Kufunga Choo
Tafuna vipande sita vya Bamia bila kutumia dawa nyigine kilasiku na Asidi ya Kujirudia rudia na kufunga choo kutakwisha, inashusha Sukari kutoka 135 hadi 98
Pumu
Bamia ina Vitamin C ambayo inawafana watoto wanaougua ugonjwa wa pumu kupumua vizuri wanapoitumia. Nusu kikombe ya Bamia iliyopikwa huwa na miligramu 13 ya vitamin C.
Kidonda Ndugu (Cancer)
Bamia husaidia kuweka Utumbo kuwa na hali nzuri hivyo kupunguza uwezakano wakuugua ugonjwa huu wa Kansa hasa kwenye utumbo mkubwa.
Mishipa midogo ya Damu Kula Bamia kwa wingi kunasaidia kuimarisha Mishipa midogo ya Damu.
Cataracts
Nusu kikombe cha Bamia iliyopikwa inakua na kiwango cha 460 IU ya vitamin A.ambayo inapunguza uwezakano wa kupata ugonjwa wa mtoto wa jicho (cataracts).
Usongo (Depression) na Kukosa Nguvu. Bamia ni mboga bora zaidi kwa wale wanaojisikia dhaifu, Kuchoka na wanao athirika na Usongo (depression).
 PIA 
1.Inasemekana ni chakula kizuri kwa watuwenye msongo wa mawazo,wanaojisikia weak n.k 
2.Ni chakula kizuri kwa wanaotaka kupunguza mwili.
3.Mbegu za bamia zina protine nyingi na mafuta
4.Inasaidia mmeng'enyo wa chakula na kupata choo vizuri
5.Zina vitamin A na C
6.Madini ya potassium,calcium na magnesium


Bamia za kukaanga na mafuta,Hapo naongeza na nyanya.


Mimi hupenda na Ugali.



Bamia za Kuchemsha[Mrenda]



Nilijua inaitwa okra lakini kumbe marekani ndio wanaita hivyo ila kwa kiingereza Ladies finger.

Kwa nini ziliitwa ladies finger?inasemekana ni kwasababu ya umbo lake lilivyo kama vidole vywa mwanamke.

Bamia hukatwa na kupikwa kwa mapishi tofauti tofauti

Ukaipika kwa urefu kwa maana ya kukata kikonyo na ncha yakekisha kuiunga na nazi.

Hizi zimewekwa tayari kwa kuokwa.Zimepasuliwa katikati halafu kwa ndani ukawekwa mchanganyiko wa vitunguu maji,jeera,coriender,pilipili ya unga,chumvi,mafuta ya kula,tangawizi na nazi vikachanganywa na kutiwa humo.Hii ni recipe ya kihindi ndio huwa wantengeneza hivi.

Huu sio mlenda bali zimekatwa ndogo ndogo zikaungwa vizuri kama zinavyoonekana...njaa inaanza kuniuma sasa maana ninavyopenda bamia.

Mlenda pale unahusika.....ukichanganya na majani ya maboga,nyanya chungu saafi unapika ladies finger zako.
 

India wanakula sana bamia....hii ni salad ambayo imetengenezwa baada ya kuziosha vizuri ladies finger zako.Unakata kikonyo unaziweka kwenye sufuria na maji kidogo halafu unazichemsha kwa dk 3 hvi ila zibaki kijani kama zilivyo.Unakatakata nyanya vidogo vidogo,vitunguu,pilipili,unati a chumvi,limao kama unavyotengeneza kachumbari.Baada ya hapo unakata bamia kama zinavyoonekana unatia hiyo salad yako tayari kuliwa.
 
Afya ni muhimu kuliko kitu chochote,ukiwa na Afya njema utafanya mambo yako yaende vizuri,hivyo basi Blog hii ya KALI YA HABARI inakuhamasisha kula bamia kwa Afya yako

0 maoni:

Chapisha Maoni