Alhamisi, 11 Agosti 2016

JESHI LA ZIMAMOTO MKOA WA PWANI LACHANGIA DAMU KATIKA HOSPITALI TEUELE YA TUMBI

Postedy by Esta Malibiche On August 11.2016

zima4 
Kamishna Jenerari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji  Thobias Andengenye akichangia damu katika moja ya matukio ya kijamii ambayo jeshi hilo limekuwa likishiriki.
………………………………………………………………………….
 damu

NA VICTOR MASANGU, PWANI
HOSPITALI teule ya rufaa ya Mkoa Tumbi  kwa sasa bado inakabikabili na changamoto ya upungufu wa damu safi na salama hivyo kupelekea  baadhi ya wagonjwa  wengine wakiwemo watoto wenye umri chini ya miaka mitano  wakinamama wajawazito, pamoja na majeruhi wa  ajali za barabarani kushindwa kupatiwa huduma ya matibabu kwa wakati muafaka.
 Kufuatia kuwepo kwa  changamoto hiyo jeshi la zimamoto na uokoaji Mkoa wa Pwani  limeamua kuendesha zoezi maalimu kwa askari wake kwa ajili ya kuweza kujitolea kuchangia damu ili kuokoa maisha ya watu wanaopoteza maisha yao kutokana na upungufu wa damu.
Akizungumza wakati wa zoezi hilo la uchangia wa damu Mratibu wa kitengo cha damu katika hospitali ya Tumbi Elisia Towo alisema kwamba  kutokana na idadi ya wagonjwa kuwa ni kubwa hivyo uhitaji ni mkubwa kwani  kwa sasa wanatumia uniti  12  mpaka  20 kwa siku ambazo bado hazijitolelezi kwa wagonjwa.
“Kwa sasa katika hospitali ya tumbi bado inakabiliwa na changamoto ya uhaba wa kuwepo kwa damu safi na salama, lakini kikubwa tunawashukuru uongozi wa jeshi la zimamoto na uokoaji Mkoa wa Pwani kwa kuamua kuitolea na kuchangia damu katika hospoitali yetu, kwa hivyo ninaomba na watu wananachi wengine wawe na moyo wakujitolea katika kusaidia,”alisema Towo.
 Aidha alisema kwamba hospitali ya tumbi imekuwa ikipokea wagonjwa wengi hivyo kunahitajika kuwepo na akiba ya uniti zaidi ya 3000 za damu kwa kipindi cha mwaka mmoja ili kuweza kukidhi mahitaji ya wagonjwa wenye mahitaji.
Kwa upande wake Kamanda wa jeshi la zimamoto na uokoaji Mkoa wa Pwani  Gudluck Zelothe alisema kwamba wameamua kuchangia damu katika hospitali ya Tumbi ili kuweza kuwasaidia wagonjwa mbali mbali  ambao baadhi yao wamekuwa wakipoteza maisha kutokana na kukosa huduma ya damu hivyo wakaona ni vema askari wake wajitolee ili kuweza kucangia.
 Naye afisa uhusianao wa jeshi la zimamoto na uokoaji Mkoa wa Pwani  Irison Mkonyi alisema nia yao kubwa ni kuhakikisha wanaweka mipango mikakati ya kuwasaidia watu amnbao wamekuwa wakipungikiwa damu kwa kuendesha zoezi la utoaji wa damu kwa kila muda wa miezi mitatu lengo ikiwa ni kuokoa maisha ya Watanania.
Naye Mhamasishaji  wa damu safi na salama katika hospitali ya Tumbi  Feliciana Mmasi amesema kwamba watoto wadogo wenye umri chini ya miaka mitano pamoja na wakinamama wajawazito wanahitaji sana  huduma ya damu safi na salama ili kuweza kuokoa maisha yao. 
 
JESHI la zimamoto na uokoaji Mkoani Pwani limeamua kuendesha zoezi la kujitolea kuchangia damu katika hospitali teule ya rufaa Mkoa tumbi kwa lengo la kuweza kupunguza vifo vinavyotokana na kukosa upatikanaji wa damu .

0 maoni:

Chapisha Maoni