Jumatano, 10 Agosti 2016

Watoto 11 waungua moto wakiwa hospitali, Baghdad


Katika tukio ambalo limewashtua watu wengi, watoto 11 wanatajwa kupoteza maisha baada ya kuungua moto wakati wakiwa katika moja ya hospitali mjini Baghdad, Iraq.
Katika taarifa imetolewa na Wizara ya Afya ya nchi hiyo, imesema kuwa tukiohilo lilitokea usiku wa Jumanne baada ya kutokea mlipuko wa moto katika chumba cha uzazi katika hospitali ya Yarmouk.
Baada ya kutokea mlipuko huo, watoto tisa na wanawake 29 waliondolewa katika hospitali hiyo na kupelekewa eneo lingine na taarifa zinaeleza kuwa chanzo cha mlipuko huo ni matatizo ya umeme

0 maoni:

Chapisha Maoni