Alhamisi, 7 Julai 2016

WAISLAMU MKOANI IRINGA WAMETAKIWA KUENDELEA KUDUMISHA AMANI NA UPENDO


MKUU wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza amewataka waumini wa dini ya Kiislam kuendelea kuhubiri amani na upendo katika taifa la Tanzania hata baada ya kumaliza kwa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani .

Masenza aliyasema hayo wakati wa futari ya pamoja ilioandaliwa na benki ya CRDB mkoa wa Iringa kwa viongozi mbalimbali wa mkoa pamoja na wateja wake wa Iringa iliyofanyika katika ofisi za CDRB juzi na kuhudhuriwa waumini wa kiislamu na wafanyabiashara mbalimbali mkoani hapa.
 Alisema kuwa jukumu la kudumisha amani na umoja miongoni mwa jamii ni jambo muhimu na linapaswa kulindwa na kila mmoja kwani amani pekee ndioyo itachangia kuletea maendeleo kwa mtu binafsi na taifa kwa ujumla.
 Aidha Masenza aliwataka wananchi kuwa walinzi kwa taifa lao na kutoa taarifa pindi wakiona kuna watu au mtu wenye nia mbaya ya kuvuruga amani au kiashirio cha ugaidi katika maeneo wanayoishi ili serikali kupitia jeshi la polisi kuweza kuwajibika kuzuia na kulinda hali itakayojitokeza.
 “Palipo na upendo watu wanaweza kuitana na kula chakula pamoja, lakini kutokana na upendo kwa wateja wake crdb wametuita hapa kwa pamoja hivyo nawaomba sana sana waumini wote wajitolee kutoa taarifa yoyote ambayo itaonekana amani yetu inataka kuteteleka” alisema
 Alisema kuwa palipo na amani kila mwananchi ataishi kwa uhuru zaidi kuliko kuonekana kuna viashiria vya uvunjifu wa amani ambapo waathirika wakubwa ni wanawake na watoto na kuwataka kudumisha amani iliyopo nchini.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa CRDB Kanda ya Iringa, Kisa Samweli amesema lengo la benki kuandaa futari kwa wateja wake ni kuimarisha umoja na wateja wao na kuwa tawi la Iringa limefikia mafanikio waliyojiwekea ikiwa ni pamoja na kukuza uchumi wa Taifa.
 Kisa alitoa rai kwa watanzania kutumia benki ya crdb katika kukopa kwa lengo la kuongeza kipato kwa wakulima, wafanyakazi na wafababiashara wakubwa na wakati ambao wanahitaji mikopo kuweza kujiendeleza kwa kuwa mikopo hiyo ina riba nafuu kwa kila mwananchi mwenye uwezo wa kukopa.
 

0 maoni:

Chapisha Maoni