Katibu
wa BAKWATA mkoa wa Singida, Alhaj Burhani Mlau, ameiomba serikali
kuangalia uwezekano wa kuiboresha adhabu (faini ) wanazotozwa madereva
kwa makosa ya kukiuka sheria za usalama barabarani, kwa madai faini
iliyopo hivi sasa ya shilingi 30,000, imefeli katika kuwaogopesha
madereva.
Amesema
ajali za barabarani ambazo nyingi zinasababishwa na uzembe, kwa sasa
zimekuwa ni wimbo wa kila siku na zinachangia Watanzania wengi kupoteza
maisha na mali zao. Kwa hiyo, zinatakiwa zitafutiwe dawa stahiki
itakayosaidia kupunguza ajali kwa kiwango cha juu.
“Dereva
wa basi la kampuni ya City Boy lililokuwa linatokea Kahama ambalo
lilihusika na ajali mbaya iliyotokea Manyoni siku chache zilizopita,
alipofika Singida alitozwa faini ya shilingi 30,000 kwa kosa la
kuendesha basi kwa mwendo kasi. Lakini baada ya kulipa faini hiyo ndogo,
aliendekeza tabia yake ya kuendesha kwa mwendo kasi na mwisho wa siku,
alisababisha idadi kubwa ya Watanzania kupoteza maisha yao,” alisema
Alhaj Mlau kwa masikitiko makubwa.
Alisema
umefika wakati sasa serikali iangalie upya uwezekano wa kutoa sheria
ambayo atawaogopesha madereva kwenda kinyume na sheria za usalama
barabarani.
“Mapendekezo
yangu adhabu kwa madereva wanaokiuka sheria za usalama barabarani,
wakipatikana na hatia, watozwe faini ya shilingi milioni tatu, wafungwe
jela miaka 30 au maisha. Kwa kifupi inatakiwa adhabu kwa watu hawa,iwe
kali zaidi,” alisema.
Akiongeza,
alisema pia umri wa dereva wanaoendesha magari ya abiri, nao uangaliwe
upya na ikiwezekana, vijana ambao maisha yao yametawaliwa na mbwe mbwe
na mihemko iliyopitiliza kama madereva wa kampuni ya mabasi ya City
Boy,wasipewe nafasi ya kuendesha magari ya abiria.
Alhaj
Mlau aliyasema hayo kwenye swala ya kusherekea Eidd Elfitri
iliyofanyika jana kwenye uwanja wa michezo wa Namfua mjini hapa.
Alhaj Mlau alitumia fursa hiyo kuwapa pole jamaa waliofiwa na ndugu zao kwenye ajali ya kugongana uso kwa uso mabasi ya kampuni moja ya City Boy na amemwomba Mungu awajalie nguvu na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu.
Alhaj Mlau alitumia fursa hiyo kuwapa pole jamaa waliofiwa na ndugu zao kwenye ajali ya kugongana uso kwa uso mabasi ya kampuni moja ya City Boy na amemwomba Mungu awajalie nguvu na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu.
Kwa
upande wake Sheikh wa mkoa wa Singida,Sheikh Salum Mahami,amewakumbusha
waumini na jamii yote ya mkoa wa Singida, kuendelea kuiombea nchi ibaki
katika amanai na utulivu ,ili waumini wa madhehebu ya dini waendelee
kuabudu kwa uhuru mpana na kujiletea maendeleo yao ya kimwili.
Alisema
amani na utulivu vikitoweka, kwanza nchi haitakalika, ustawi wa
madhehebu ya dini utakuwa shakani na mbaya zaidi, maendeleo ya kijamii
hayatakuwepo.
“Maombi
haya ya kuiombea nchi yetu, yaendelee sambasamba na kumwombea rais wetu
Dk.Magufuli na watendaji wengine wa ngazi mbalimbali ili Mungu awape
nguvu na afya, kwa ajili ya kuwatumikia vema wananchi,” alisema.
Na Nathaniel Limu, Singida






0 maoni:
Chapisha Maoni