Katibu
Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Prof. Justin Ntalikwa wa kwanza
kulia, akifuatiwa na Kamishna Msaidizi anayeshughulikia masuala ya
Petroli Mwanamani Kidaya (katikati) na Mratibu wa Mradi, Salum Mnuna
(kushoto) wakifuatilia majadiliano wakati wa kikao cha Makatibu Wakuu
wa nchi za Uganda na Tanzania, kilichohusu utekelezaji wa Mradi wa bomba
la Mafuta ghafi kutoka Hoima nchini Uganda hadi Bandari ya Tanga,
Tanzania.
Kikao
hicho kilifanyika tarehe 04.07.2016, kabla ya kikao cha Mawaziri wan
chi husika. Aidha, Wataalam wengine (hawapo pichani) waliohudhuria kikao
hicho kwa upande wa Tanzania walitoka Wizara ya Nishati na Madini,
Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) na Mamlaka ya Bandari
Tanzania (TPA).
Pia,
kwa upande wa Uganda waliwakilishwa na Wizara ya Nishati na Maendeleo ya
Madini, wadau wa sekta hizo kutoka idara mbali mbali za Serikali na
wawekezaji kampuni za Total, CNOOC na Tullow.
Vikao
hivyo ni sehemu ya Maandalizi ya ripoti iliyowasilishwa katika kikao
cha Mawaziri cha tarehe 5.07.201, Hoima nchini Uganda.
Waziri
wa Nishati na Madini (katikati mstari wa kwanza kulia) akiongoza
Wataalam wa Watanzania katika kikao cha Mawaziri wa Tanzania na Uganda
kujadili utekelezaji wa Mradi wa bomba la Mafuta kutoka Hoima nchini
Uganda hadi Bandari ya Tanga. Kikao cha Mawaziri kimefanyika tarehe
5.07.2016.
0 maoni:
Chapisha Maoni