Waziri
wa Nishati na Madini Mhe.Prof Sospeter Muhongo amesema kuwa uwekezaji
wa umeme Vijijini awamu ya tatu utagharimu zaidi ya Trilioni moja.
Waziri
Prof. Muhongo ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati akizindua
mpango wa Nishati endelevu kwa wote (SE4ALL) wenye lengo la kuhakikisha
upatikanaji wa nishati ya uhakika kufikia mwaka 2030.
“Mpango
huu umelenga kufanikiwa mwaka 2030, lakini kwa sisi Tanzania kabla ya
mwaka huo tutakuwa na umeme kwa kila mtanzania na Programu hii
italifanya taifa letu lijulikane dunia kwani tuna dhamira ya kumfanya
kila mtu apate umeme,KWANI utasaidia suala la ajira na kutokomeza
umaskini, kwaiyo kama nchi tuko katika ngazi za juu za huu mradi katika
kuufanikisha tukishirikiana na wadau mbalimbali”Alisema Prof Muhongo.
Waziri
wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo akizungumza na wadau wa
Nishati na Madini(hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa mpango wa
Nishati endelevu kwa wote wenye lengo la kuhakikisha upatikanaji wa
nishati ya uhakika kufikia mwaka 2030 katika viwanja vya Mwalimu Nyerere
jijini Dar es Salaam.
Aidha
alisema kuwa Programu hii ya Umoja wa Mataifa itasaidia sana katika
kuongeza vyanzo vya kuzalisha umeme kwani inafanana sana na ile ya kwetu
ya Taifa ambapo tutazalisha umeme mwingi kutokana na Gesi, Makaa ya
Mawe,Umeme wa maporomoko ya Maji, Umeme wa Jua, Joto Ardhi na Mabaki ya
mimea na kwa hivi tutafanikisha kujenga nchi ya viwanda kwa sababu tuna
miradi ambayo itahakikisha uwepo wa umeme wa uhakika kwa ajili ya uchumi
wa Taifa letu.
Amesema
mashirika mengi yamesaidia katika kufanikisha upatikanaji wa umeme
vijijini ikiwemo benki ya Dunia ambayo imetoa dola milioni 200, Umoja wa
Ulaya umetoa euro 180, Nchi za Nordic zimetoa dola milioni 300 pamoja
na Benki ya Maendeleo ya Afrika nayo imetoa fedha katika kuwekeza kwenye
umeme vijijini pia.
Waziri
wa Nishati na Madini Prof Sospeter Muhongo akikata utepe kuzindua
mpango wa Nishati endelevu kwa wote (SE4ALL) wenye lengo la kuhakikisha
upatikanaji wa nishati ya uhakika kufikia mwaka 2030 jijini Dar es
Salaam.Kushoto kwake ni Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa
na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa(UNDP), Alvaro
Rodriguez.
Waziri
wa Nishati na Madini Prof Sospeter Muhongo akionyesha jarida maalum
wakati wa uzinduzi wa mpango wa Nishati endelevu kwa wote (SE4ALL)wenye
lengo la kuhakikisha upatikanaji wa nishati ya uhakika kufikia mwaka
2030.Kushoto kwake ni Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na
mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) Bw.Alvaro Rodriguez (UNDP) na
Kulia ni Mwakilishi Mkazi wa benki ya Maendeleo ya Afrika Bi.Tonia
Kandiero.
Baadhi
ya Wadau mbalimbali wa Nishati na Madini wakimsikiliza Mhe.Prof
Sospeter Muhongo jijini Dar es Salaam katika uzinduzi wa mpango wa
Nishati endelevu kwa wote (SE4ALL) wenye lengo la kuhakikisha
upatikanaji wa nishati ya uhakika kufikia mwaka 2030.
Waziri
wa Nishati na Madini Prof Sospeter Muhongo akiwa katika picha ya pamoja
na wadau mbalimbali kutoka Umoja wa Mataifa,Benki ya Maendeleo ya
Afrika na Umoja wa Ulaya baada ya uzinduzi wa mpango wa Nishati endelevu
kwa wote(SE4ALL) wenye lengo la kuhakikisha upatikanaji wa nishati ya
uhakika kufikia mwaka 2030.
0 maoni:
Chapisha Maoni