Fainali
ya mashindano ya tenesi ya Wimbledon kwa upande wa anawake imamalizika
kwa Mmarekani, Serena Williams kuibuka mshindi baada ya kumfunga
Mjerumani, Anelique Kerber.
Serena
amefanikiwa kushinda taji hilo kwa kumfunga Angelique seti 7-5 na 6-3,
ushindi ambao umemfanya kuendelea kujiwekea historia katika mashindano
makubwa ya tenesi ambayo amekuwa akishiriki.
Baada
ya kushinda taji hilo, sasa ameweka historia mpya baada ya kufikisha
mataji saba ya Wimbledon lakini kama hilo halitoshi amevunja rekodi ya
Steffi Graf ya kushinda mataji makubwa ‘Grand Slam’ baada ya kufikisha
idadi aliyokuwa nayo mchezaji tenesi huyo ya kuwa na mataji 22.
Pamoja
na kuweka rekodi hizo mbili ambazo hazikuwepo awali lakini unapaswa
kufahamu kuwa Serena Williams ndiyo anaongoza katika orodha ya wachezaji
bora wa tenesi kwa upande wa wanawake.
0 maoni:
Chapisha Maoni