Jumamosi, 9 Julai 2016

Naibu Waziri wa Afya Dk. Kigwangalla azindua rasmi Shirika la Afya na Elimu ya Tiba (TAHMEF) Jijini Dar


Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dk. Hamisi Kigwangalla  jioni ya jana Julai 8.2016, amezindua rasmi Shirika la Afya na Elimu ya Tiba (TAHMEF)  inayojishughulisha na masuala ya Afya Nchini Tanzania sambamba na kuzindua Programu maalum ya “NURU YA AFYA”.
Tukio hilo ambalo Dk. Kigwangalla alikuwa mgeni rasmi, pia lilienda sambamba na uzinduzi wa mpango maalum wa kutoa elimu na tiba ujulinakanao kama “NURU YA AFYA” ambapo mpango huo unatarajia kuanza  kwa Wilaya ya Bagamoyo kwa kuweka kambi maalum na kutoa huduma mbalimbali za kiafya pamoja na  elimu huku lengo likiwa ni kuwafikia watu zaidi ya 500 kwa kila baada ya miezi mitatu.
Awali akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Dk. Kigwangalla alipongeza juhudi za taasisi binafsi kwa namna zinavyojitolea kuisaidia Serikali katika mapambano hivyo wataendelea kuziunga mkono kwa hali na mali.
“Naomba nichukue fursa hii kuwashukuru kwa kuanzisha kitu kama hiki kwani ni jambo jema na munaisaidia Serikali katika kufikia malengo yake. Naamini shirika kama hili TAHMEF ambapo wengi wenu ni vijana na wasomi hasa katika kada ya Afya ni chachu kubwa sana ya kufikia malengo katika sekta ya Afya ya Nchini.
Watu wengi wanaamini Serikali pekee yake ndio wenye jukumu la kutatua matatizo katika Sekta ya Afya. Bali suala hili ni letu sote hivyo kwa uwepo wenu ni fursa ya kipekee kwa nanyi kusaidiana na Serikali katika kufikia malengo yake,” alieleza Dk. Kigwangalla katika uzinduzi huo.
Hata hivyo Dk. Kigwangalla alieleza kuwa,  Vijana hao wameonyesha uthubutu ambapo amewatakia kila la kheri katika shughuli zao hizo.
Aidha, Dk. Kigwangalla pia aliweza kuendesha harambee ndogo ya kusaidia taasisi hiyo na watu mbalimbali waliweza kujumuika kuichangia.
Kwa upande wake, Mwenyekiti na Mwanzilishi wa Shirika la Afya na Elimu ya Tiba (TAHMEF), Bi.Juliana Busasi alieleza kuwa wakiwa kama vijana wamekuwa na malengo makubwa ya kusaidiana na Serikali hasa katika Afya hivyo amemuhakikishia Naibu Waziri wa Afya kuwa, shirika lao itafanya kazi bega kwa bega na Wizara yake pamoja na wadau wengine katika kufikia malengo yaliyopo hapa nchini.
Nae Mkurugenzi wa Miradi wa shirika hilo, Hansi Olomi amebainisha kuwa, ili kufikia malengo, TAHMEF  inatarajia kuendesha miradi mbalimbali ambapo wataanza na mradi wa “NURU YA AFYA” ambao unatarajia kuanza Bagamoyo Mkoani Pwani kuanzia Mwezi Oktoba Mwaka huu.
Mradi huo wa Nuru Yetu, ni  miongoni mwa miradi ya shirika hilo ambapo watakuwa wakitoa huduma ya Afya na Elimu kwa watu mbalimbali hapa nchini ambapo kwa kuanzia wataanza na Wilaya ya Bagamoyo.
Shirika hilo ya TAHMEF inaundwa na vijana wanaosomea kada ya Udaktari katika vyuo vya tiba hapa nchini ikiwemo wale wa Hubert Kairuki, Muhimbili pia wapo kutoka Chuo kikuu cha Mlimani (UDSM) na wengineo.
DSC_9506 DSC_9508Mwenyekiti wa baraza la chuo Kikuu cha Tumaini Makumira, Prof. Esther Mwaikambo, (Pichani Juu) akisalimiana na Dk. Kigwangalla  wakati alipowasilia katika ukumbi wa mikutano uliopo katika hoteli ya Seashells Milllennium Hotell-LAPF Tower Jijini Dar es Salaam
DSC_9513Edmond Issae wa taasisi ya TAHMEF akitoa neno fupi la ufunguzi wa tuko hilo, Kulia ni  Kijanana Willson ambaye alikuwa MC.
DSC_9649Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dk. Hamisi Kigwangalla akifuatilia uzinduzi huo wa taasisi ya TAHMEF
DSC_9516Mwenyekiti na Mwanzilishi wa Shirika la Afya na Elimu ya Tiba (TAHMEF), Bi.Juliana Busasi akitoa maelezo mafupi juu  ya shirika hilo kwa wageni waalikwa (hawapo pichani)
DSC_9525 DSC_9526Kiongozi wa Miradi ya shirika hilo la TAHMEF,  Hans Olomi akielezea namna walivyojipanga kuendesha miradi yao kwa njia ya kitaalam ikiwemo kutumia ujuzi wao katikak Sekta ya Afya
DSC_9529Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dk. Hamisi Kigwangalla akizindua rasmi shirika la TAHMEF.
DSC_9615Meza kuu
DSC_9636Wageni waalikwa wakiwa meza kuuDSC_9565Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangalla akitoa hutuba fupi ya uzinduzi huo.
DSC_9530Dk. Kigwangalla akitoa maelezo namna Serikali inavyojitahidi kusaidia Sekta ta Afya hapa nchini huku wakiimiza wadau kuwa mstari wa mbele kusaidiana nayo.
DSC_9625Baadhi ya wanachama wa Shirika la Afya na Elimu ya Tiba (TAHMEF) pamoja na wageni wengine waalikwa.
DSC_9631Mchora vibonzo maarufu na Mhariri wa katuni wa ITV, Bwana Nathan Mpangala akifuatilia kwa umakini uzinduzi huo. Nathan ni miongoni mwa wadau wa shirika la TAHMEF.
DSC_9632 DSC_9628Wageni waalikwa.
DSC_9635 DSC_9637Mwenyekiti wa baraza la chuo Kikuu cha Tumaini Makumira, Prof. Esther Mwaikambo (kushoto) akiwa pamoja na  Bi. Kokushubira Kairuki ambaye ni Mwenyekiti wa Hubert Kairuki University  wakifuatilia tukio hilo. Miongoni mwa vijana walioanzisha shirika hilo ni wanafunzi wa udaktari katika chuo hicho cha Kairuki
DSC_9572Nathan Mpangala akitoa ahadi yake katika harambee fupi ya kuchangia mradi wa NURU YA AFYA wa  shirika la  TAHMEF.
DSC_9647Moja ya picha iliyokuwa ikinadiwa katika harambee hiyo.
DSC_9571Nathan akisalimiana na Naibu Waziri wa Afya, Dk. Kigwangalla
  DSC_9584Dk. Kigwangalla akieleza jambo kwa Pastor Maestro ambaye pia ni Naibu Mkurugenzi wa CDC
DSC_9589Bi. Kokushubira Kairuki ambaye ni Mwenyekiti wa Hubert Kairuki University akitoa ahadi ya kuchangia shirika la TAHMEF
DSC_9601Wageni waalikwa kutoka Mamlaka ya Mawasiliano wakiahidi kuchangia shirika la TAHMEF
DSC_9609Wageni waalikwa kutoka Mamlaka ya Mawasiliano wakiahidi kuchangia shirika la TAHMEF
DSC_9655Dk. Kigwangalla akipokea picha ya mchoro ambayo ilitolewa kwake baada ya kuinunua kwa Sh. Milioni moja na nusu katika Harambee ya kuchangia shirika la TAHMEF
DSC_9656Pastor Maestro akipokea picha ambayo aliichangia katika Harambee hiyo
DSC_9659Dk. Kigwangalla akpokea keki maalum ambayo alikabidhiwa kama zawadi kwa mchango wake wa kuthamini shughuli za taasisi binafsi katika mchango wa kufikia malengo kwenye sekta ya Afya.
DSC_9662Dk. Kigwangalla akpokea keki maalum ambayo alikabidhiwa kama zawadi kwa mchango wake wa kuthamini shughuli za taasisi binafsi katika mchango wa kufikia malengo kwenye sekta ya Afya.
DSC_9753Mwenyekiti na Mwanzilishi wa shirika laTAHMEF, Bi.Juliana Busasi akimshukuru mgeni rasmi kwa kuzindua rasmi taasisi hiyo.
DSC_9667Dk. Kigwangalla akikata keki maalum 
DSC_9672Dk. Kigwangalla akimlisha keki Bi. Kokushubira Kairuki ambaye ni Mwenyekiti wa Hubert Kairuki University
DSC_9674Dk. Kigwangalla akimlisha keki  Mwenyekiti wa Baraza la chuo Kikuu cha Tumaini Makumira, Prof. Esther Mwaikambo.
DSC_9675Dk. Kigwangalla akimlisha keki Pastor Maestro.
DSC_9677Dk. Kigwangalla akimlisha keki Mwanzilishi na Mwenyekiti wa shirika la TAHMEF, Bi. Juliana Busasi
DSC_9692 DSC_9695Pia kulikuwa na burudani kidogo….
DSC_9630Wageni waaliwa wakifuatilia tukio hilo
DSC_9697 DSC_9701Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dk. Hamisi Kigwangalla akipata picha na wageni wengine waalikwa pamoja na viongozi wa shirika la TAHMEF 
DSC_9706 DSC_9713Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangalla akipata picha na baadhi ya viongozi wa TAHMEF.
  DSC_9719 DSC_9723 DSC_9726 DSC_9730Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangalla  akipata picha na baadhi ya vijana wanaosomea kada  Udaktari ambao walialikwa katika tukio hilo
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangalla  akipata picha na baadhi ya vijana wanaosomea kada  udaktari ambao walialikwa katika tukio hilo
DSC_9745Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dk. Hamisi Kigwangalla akipata picha ya ukumbusho na wanafunzi wanaosomea Udaktari hapa Nchini.
DSC_9747Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dk. Hamisi Kigwangalla akipata picha ya ukumbusho na wanafunzi wanaosomea Udaktari hapa Nchini
DSC_9772Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangalla akipata picha ya ukumbusho na wanafunzi wanaosomea Udaktari hapa Nchini
DSC_9757Profesa Mwaikambo akipata picha ya pamoja na Juliana.
DSC_9742Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangalla akipata ‘selfie’ na  picha ya ukumbusho na wanafunzi wanaosomea Udaktari hapa Nchini ambao wameamua kuanzisha taasisi ya kusaidia jamii katika sekta ya Afya ijulikanayo kama TAHMEF. (Picha zote na Andrew Chale,

0 maoni:

Chapisha Maoni