Baada
ya Uingereza kutolewa katika michuano ya Euro na kumfukuza aliyekuwa
kocha wake, Roy Hodgson na kuanza kutajwa baadhi ya makocha wanaoweza
kukabidhiwa mikoba ya kocha Hodgson, mmoja wapo ni kocha wa Arsenal,
Arsene Wenger ambaye na yeye ameonyesha nia ya kuifundisha timu ya taifa
ya Uingereza.
Mbali
na maelezo ambayo ameyatoa kocha huyo kuwa Uingereza inafuatia kuwa
nyumbani kwake baada ya Ufaransa lakini pia kumekuwepo na taarifa za
chini ya kapeti kuwa kocha huyo hana uhakika kama ataongezewa mkataba na
Arsenal pindi utakapomalizika mwakani 2017.
Akizungumza
na kituo cha michezo cha beIN Sports, Wenger alisema “Nikitakiwa
kuiongoza Uingereza? Kwanini nikatae? siwezi kulipinga hilo, lakini nina
furaha kuongoza klabu,
“Uingereza ni nchi yangu ya pili, nilishangazwa na Uingereza kutolewa na Iceland, sikuamini hilo,” alisema Mourinho na kuongeza.
“Ukiangalia
mchezo wao unaweza kupata picha jinsi ilivyo, baada ya dakika ya 60
kama kuna vitu vibaya vimewapata, walikuwa wamechanganywa na mchezo au
wamechoka? Sijui lakini Uingereza wanatakiwa kutafuta jawabu kwa
kilichowatokea dhidi ya Iceland”
0 maoni:
Chapisha Maoni