Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan
amewahimiza watendaji wa Mradi wa Jukwaa la Kijani la wanawake Nchini
wahakikishe wanaendelea na mkakati wa kuelemisha wanawake kuhusu namna
ya kukukabiliana na mabadiliko ya Tabia hapa Nchi.
Makamu
wa Rais SAMIA SULUHU HASSAN ametoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam
wakati anazindua mradi wa GREEN VOICES, mradi unaolenga kusaidia
wanawake kukabiliana na mabadiliko ya Tabia, unaofadhiliwa na Rais wa
Mfuko wa Wanawake Barani Afrika Maria Teresa Fernandez De la vega
Makamu
wa Rais pamoja na kupongeza jitihada zinazofanywa na Jukwaa hilo katika
kusaidia wanawake kupambana na mabadiliko ya Tabia ya nchini, amesema
bado upo umuhimu mkubwa kwa wanawake kuelimishwa zaidi kuhusu
mabadiliko hayo kwa sababu wao ni moja ya kundi ambalo linaguswa na
mabadiliko ya tabia ya nchi ikiwemo suala la ukame.
Amesema
Bara la Afrika linapoteza mabilioni ya dola kutokana na mabadiliko ya
Tabia ya Nchi ikiwemo tatizo la ukame ambao umechangia kupunguza
uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara kwa kiasi kikubwa pamoja na
uhaba wa maji.
Makamu
wa Rais SAMIA SULUHU HASSAN amesema nchi za Afrika bado zinakabiliana
uhaba wa kifedha,taarifa sahihi na teknolojia katika jitihada za
kupambana ipasavyo na mabadiliko ya tabia ya nchini.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan
akihutubia wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Green Voices Tanzania
uliofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan
akipata maelezo namna ya mkaa wa karatasi unavyofanya kazi kutoka kwa
Mkurugenzi wa kampuni ya Mchau Windmill Ndugu Laurian Mchau wakati wa
uzinduzi wa mradi wa Green Voices Tanzania.
Cake ya Muhogo.
Mkaa wa Karatasi.
Makamu wa Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipata maelekezo ya
namna zao la muhogo linavyoweza kuwa na idadi nyingi ya vyakula.
Mshauri
na Mjumbe wa Bodi ya Mfuko wa Wanawake Barani Afrika Mhe. Getrude
Mongella akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi wa Green Voices
Tanzania uliozindiliwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.
0 maoni:
Chapisha Maoni