Siku
chache zilizopita Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,
Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangalla aliweka video katika ukurasa
wake wa Twitter kuwa ikimuonyesha akizungumzia taasisi ambazo zimekuwa zikihamasisha watu kushiriki mapenzi ya jinsia moja na kuwa serikali itazichukulia hatua za haraka ikiwa ni pamoja na kuzifuta.
Baada
ya taarifa hiyo, Mo Blog ilipata nafasi ya kuzungumza na Dk.
Kigwangalla kuhusu hatua ambazo serikali kupitia wizara ya afya
inazifanya ili kuzichukulia hatua taasisi zote zinazosaidia watu
wanaoshirikia mapenzi ya jinsia moja.
Dk.
Kigwangalla alisema wameanza taratibu za kuzichukua hatua taasisi hizo
kwa kukutanisha wataalam kutoka wizara mbalimbali ili kufanya kazi ya
kuchambua kazi zinazofanywa na kila taasisi ikiwa ni pamoja na kutoa
mapendekezo ya adhabu ambazo zitachukuliwa kwa taasisi hizo.
“Tumeanza
kuchukua hatua na wataalam wa wizara yetu wameungana na wataalam kutoka
wizara nyingine ambazo ni Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Jeshi
la Polisi kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani na Ofisi ya Waziri Mkuu na
watakuwa katika kamati moja wakijadili kuhusu jambo hilo,
“Kamati
hii inakazi ya kupitia sera na sheria na baada ya hapo watatoa
mapendekezo ya hatua ambazo zitachukuliwa lakini bado hatujayaweka wazi
na tutajumuisha na lile ambalo nilisema Mwanza (video aliyoweka Twitter),” alisema Dk. Kigwangalla.
Naibu
waziri huyo wa wizara ya afya alisema baada ya mapendekezo ya adhabu,
kamati itapitia miradi yote ambayo imeombwa kufanyika kupitia wizara ya
afya ili kuifahamu miradi inayojishughulisha kuwasaidia mashoga na
kuhamasisha watu kushiriki mapenzi ya jinsia moja.
“Kuna
taasisi zikituletea maombi zinakuwa zinaomba vitu vingine wa
wanavyofanya ni vitu vingine, kamati itapitia tena miradi inayoombwa
kwetu wizara ya afya na taasisi zote ambazo zitakutwa zinahamasiha
mapenzi ya jinsia moja zitapewa adhabu ambazo zimetolewa mapendekezo,
“Sijui
ni lini watamaliza kazi ya kuzichambua taasisi hizo maana kazi hiyo ni
kubwa sababu watapitia mradi mmoja mmoja baada ya hapo taasisi
zitakazokuwa zinafanya harakati za kufanyika kwa vitendo hivyo
zitachukuliwa hatua na katika hilo tutakuwa serious nchi yetu ina sheria
yake na maadili yake,, tutatekeleza hilo,” alisema Dk. Kigwangalla.
0 maoni:
Chapisha Maoni