DEREVA
wa basi la City Boys T.247 BCD Jeremia Martini Sempungwe (33) mkazi wa
Kinondoni jijini Dar-es-salaam, jana amepandishwa kizimbani katika
mahakama ya hakimu mkazi mjini Singida, kwa tuhuma ya makosa 30 ya
kusababisha vifo vya abiria 30 bila kukusudia.
Awali
Hakimu wa Mahakama hiyo, Joyce Minde, alimwarifu mshitakiwa kuwa
atasomewa makosa yake yote na ayasikilize kwa makini. Lakini hatajibu
chochote kwa madai kwamba mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikilza kesi
za mauaji.
Baada
ya hapo, Mwendasha mashitaka wakili wa serikali mkuu mfawidhi mkoa wa
Singida, Zakaria Ndaskoi, alisema kuwa mshitakiwa anashitakiwa kwa kosa
la kwenda kinyume na kifungu 195 na 198 cha kanuni ya adhabu sura 16
toleo la kwanza kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2002.
Akifafanua,
alisema siku ya tukio basi lililokuwa likiendeshwa na mshitakiwa
Jeremia likitokea Kahama likielekea jijini Dra-es-salaam, lilipofika
eneo la tukio liligongana uso na basi jingine la kampuni hiyo hiyo ya
City Boys.
Dereva
wa basi la kampuni ya City Boys, Jeremia Martin Sempungwe (33) mwenye
begi mkononi, akisindikizwa mahakamani na askari polisi, kujibu tuhuma
ya mauaji ya bila kukusudia.
“Mheshimiwa
hakimu baada ya mabasi hayo kugongana,yalisabaisha abiria 30 kupoteza
maisha na kujeruhi wengine 54 vibaya. Kutokana na mazingira
yaliyosabaisha vifo hivyo na majeruhi, kumepelekea mshitakiwa ashitakiwe
kwa kosa la kuuawa bila ya kukusudia”,alisema wakili huyo mfawidhi wa
serikali.
Zakaria
aliiambia mahakama hiyo iliyofurika umati wa wasikilizaji, kwamba
upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilkia na pia mshitakiwa dereva
mwingine wa basi T.531 DCE Boniface Mwakalukwa, bado anaendelea kusakwa,
ili akamatwe na kufikishwa mahakamani.
Baada
ya kusema hayo,wakili wa kujitegemea mjini Singida, Francis Kitope,
alisimama na kuiomba mahakama hiyo impe mteja wake dhamana, kwa madai
kuwa kesi hiyo inadhaminika.
Kutokana
na ombi hilo,wakili wa serikali Zakaria alisimama na kupinga mshitakiwa
asipewe dhamana akidai kuwa wakati huu si salama kwa mshitakiwa kuwa
huru kwa vile tukio bado bichi na ndugu za abiria waliofariki na wale
waliojeruhiwa,bado wana uchungu mkubwa.
Dereva
wa basi la kampuni ya City Boys,Jeremia Martin Sempungwe (33) (kulia),
akiwa kwenye korido la Mahakama ya Hakimu mkazi mjini Singida, akielekea
kwenye chumba cha mahakama kusomewa makosa yanayomkabili ya kuuawa
abiria 30 bila kukusudia. Hata hivyo,mshitakiwa hakutakiwa kujibu
chochote kwa vile mahakama hiyo, haina mamlaka ya kusikiliza kesi za
mauaji.
“Si
hivyo tu,washitakiwa wengine wametoroka bado hawajakamatwa wanaendelea
kusakwa.Mshitakiwa akipewa dhamana, ataathiri shauri letu”,alisema
Zakaria ambaye alikuwa akisaidiwa na Petrida Muta.
Baada
ya mabishano hayo,hakimu Minde aliagiza upande wa jamhuri ukaandike
pigamizi kwa maandishi, na kisha kuliwasilisha mahakamani ili mahakama
iweze kutoa maamuzi.
Kesi hiyo inatarajiwa kutajwa tena Julai 21 mwaka huu.
Katika
hatua nyingine, Kamanda wa Jeshi la polisi mkoa wa Singida, ACP Thobias
Sedoyeka, amemtaka dereva Boniface Mwakalukwa aliyefanikiwa kutoroka,
ajisalimishe haraka,vinginevyo akikamatwa na polisi atapata adhabu kali
zaidi.
Dereva
wa basi la kampuni ya City Boys, Jeremia Martin Sempungwe (33) (mwenye
jaketi) akiwa kwenye chumba cha mahakama tayari kusomewa makosa yake 30
ya kuuawa abiria 30 bila ya kukusudia.
Katika
tukio jingine,Sedoyeka alisema watu wanne wamefariki dunia baada ya
lori aina ya scania T.716 MMM lililokuwa likivuta tela T.391 DCY
linalomilikiwa na kampuni ya Hascam Investment and General Supplies
LTD,ya jijini Dar-es-salaam, kutumbukia darajani katika mlima wa
Sekenke wilaya ya Iramba.
Aliwataja
watu hao waliofariki julai saba mwaka huu saa tatu usiku,kuwa ni
Thabias Alli (dereva wa lori hilo),wafanyabiashara wa Igunga Christopher
Kilindiro (30)na Rajabu Shaban (25) na mwanaume mmoja ambaye
hajatambulika.
Aidha,alitaja
majeruhi wa ajali hiyo kuwa ni Lausius Charles Haule (15) mwanafunzi wa
darasa la saba shule ya msingi Igunga na Marwa Charles (37)
mfanyabiashara wa Igunga,wote wamelazwa katika hospitali ya wilaya ya
Iramba.
Sedoyeka alisema chanzo cha ajali hiyo ni kufeli kwa breki za lori hilo.
Imeandikwa na Nathaniel Limu, Singida
Dereva
wa basi la kampuni ya City Boys, Jeremia Martin Sempungwe (33) akiwa na
wakili wake wa kujitegemea Francis Kitope wakiweka mambo sawa kabla
mshitakiwa kupandishwa kizimbani.
Mwendesha
mashitaka wakili wa Serikali Mkuu Mfawidhi mkoa wa Singida, Zakaria
Ndaskoi,akitoa ufafanuazi kwa waandishi wa habari juu ya amri ya
mahakama ya kutaka wakaandike zuio la kutaka mshitakiwa asipewe dhamana.
0 maoni:
Chapisha Maoni