Jumatano, 17 Agosti 2016

KITUO CHA UWEKEZAJI (TIC) CHATETA NA WAHARIRI WA VYOMBO VYA HABARI LEO

01
Kaimu Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania TIC Bw. Clifford Tandari akifungua semina ya Wahariri wa Vyombo vya habari kuhusu shughuli mbalimbali zinazofanywa na kituo hicho katika masuala mbalimbali ya uwekezaji na jinsi ambavyo kimekuwa kikishughulikia na kurahisisha sekta ya uwekezaji na wawekezaji kusajiliwa kwa haraka zaidi ili kuendelea na shughuli zao ikiwa ni juhudi za kuhakikisha uwekezaji wa haraka na salama.
Juhudi hizi za  TIC pia ni  kuunga mkono juhudi za Mh. Rais Dk John Pombe Magufuli kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda vidogo na  vya kati na kuleta maendeleo na uchumi imara kwa watanzania.
Kaimu Mkurugenzi huyo ameviomba vyombo vya habari mbalimbali hapa nchini kufanya kazi kwa karibu na Kituo cha Uwekezaji cha TIC ili kuelimisha wananchi na wageni mbalimbali wenye nia ya kuja kuwekeza hapa nchini. Semina hiyo imefanyika kwenye ofisi za kituo hicho jijini Dar es salaam leo.
1
Kaimu Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania TIC Bw. Clifford Tandari akisisitiza jambo katika semina hiyo wakati akifungua semina ya Wahariri wa vyombo vya habari katika semina iliyofanyika kwenye ofisi za kituo hicho.
2
Kaimu Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania TIC Bw. Clifford Tandari akizungumza jambo na wahariri wa vyombo vya habari mara baada ya kufungua semina hiyo.
3
Pendo Gondwe Meneja Uhusiano wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania TIC akifafanua jambo wakati semina hiyoikiendelea.
4
Mkurugenzi wa Uwekezaji Bw. John Mnali akitoa mada kwa waandishi wa habari wakati semina hiyo ikiendelea.
5
Wakuu wa vitengo mbalimbali Kituo cha Uwekezaji TIC Tanzania kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Uwekezaji na Uwezeshaji Nakuala Senzia, Mkurugenzi wa Uwekezaji  TIC Bw.John Mnali na Mkurugenzi wa Utafiti na Mfumo wa Mawasiliano Bw. Ayubu Sizya.
6
Baadhi ya washiriki wa semina hiyo wakifuatilia mada mbalimbali zilizotolewa na watoa mada kutoka TIC.
78
Mkurugenzi wa Uwekezaji na Uwezeshaji Nakuala Senzia akizungumza akitoa mada kuhusu uwekezaji na taratibu zake wakati semina hiyo ikiendelea katika ofisi za Kituo cha Uwekezaji Tanzania TIC leo.
9
Mkurugenzi wa Utafiti na Mfumo wa Mawasiliano Bw. Ayubu Sizya akitoa mada katika semina hiyo, kulia ni Mkurugenzi wa Uwekezaji na Uwezeshaji Nakuala Senzia  na katikati ni Mkurugenzi wa Uwekezaji TIC Bw.John Mnali.

0 maoni:

Chapisha Maoni