Aliyekuwa
Rais wa zamani wa Shirikisho la mpira wa miguu duniani FIFA, Joao
Havelange ambaye amefariki jana kutokana na kusumbuliwa kwa muda mrefu
na ugonjwa wa mapafu akiwa Rio De Janeiro huko nchini Brazil alifanya
mengi katika uongozi wake na hata kipindi akiwa hayupo madarakani na
jambo kubwa zaidi ni kuwezesha Olimpiki ya Rio 2016 kufanyika nchini
kwake.
Havelange
aliyemuachia kijiti Sepp Blatter alikuwa Rais wa saba kuongoza
Shirikisho hilo kwa muda wa miaka 24 tangu Mei 8 1974 hadi Juni 8 1998
na amefariki akiwa na umri wa miaka 100 tangu alipozaliwa mwaka 1916 May
8 nchini Brazil
Atakumbukwa
na mambo mengi aliyoyafanya katika kukuza na kusaidia mpira wa miguu
kwa muda wake wote aliokuwa madarakani kwa kuhakikisha kanuni na sheria
zote zinafuatwa vizuri kuanzia katika uongozi na hata mambo mbalimbali
yanayohusu soka kila kona ya dunia.
Akiwa
na elimu ya Sheria, Jina lake lilizidi kuwa kubwa pale alipoongeza
washiriki katika kombe la dunia kutoka timu 16 hadi kufikia timu 32
ambapo mashindano ya 6 yalifanyika chini ya Utawala wake.
Havelange
aliiwakilisha Brazil katika mashindano ya Olimpiki ya kuogelea mwaka
1936, mwaka ambao aliidhinishwa kuwa mwanasheria kabla ya kuchaguliwa na
IOC, Lakini pia alikuwa mmoja kati ya wanakamati wa Olimpiki kuanzia
mwaka 1963 hadi 2011 alipojiuzulu kutokana na matatizo ya kiafya.
Alijiuzulu
pia nafasi ya Urais wa FIFA April mwaka 2013 kufuatia uchunguzi
uliokuwa umefanywa na kutoa ripoti ya madai ya kupokea rushwa na mwaka
uliofuatia alilazwa hospitalini kufuatia kukumbwa na ugonjwa wa mapafu.
Joao
Havelange ambaye jina lake ni Jean-Marie Faustin Godefroid De Havelange
alikuwa alikuwa na ndoto ya siku nyingi kuhakikisha Olimpiki itafanyika
kwa nguvu zake nchini Brazil na jambo hilo alilifanikisha ingawa
alikuwa amekwishaanza kuumwa.
Na Derick Highiness
0 maoni:
Chapisha Maoni