Waziri
wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu
ametoa rai kwa jamii kupiga vita mila na tamaduni potofu zinazosababisha
kuwepo kwa tatizo la ukatili wa kijinsia kwa watoto wa kike wenye umri
kati ya miaka 13 hadi 18.
Mhe.
Ummy Mwalimu ametoa rai hiyo wakati alipokuwa akizindua maadhimisho ya
siku ya idadi ya watu duniani iliyofanyika katika Viwanja vya Mnazi
Mmoja Jijini Dar es Salaam ambapo pamoja na mambo mengine ameiomba jamii
na Mashirika mbalimbali yasiyo ya kiserikali kushirikiana kwa pamoja
kutokomeza mila hizo.
Amesema
kuwa kuwa mfumo dume ndio changamoto kubwa inayowakwaza watoto wa kike
kuanzia ngazi ya kaya ambapo kazi za ndani kama za kuosha vyombo,
kufagia na kuhudumia nyumba kwa ujumla hufanywa na mtoto wa kike, hali
hiyo humpotezea muda mtoto wa kike hatimae kupunguza ushiriki wake
katika elimu na mambo mengine ya maendeleo.
Mwakilishi
wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya Watu Duniani
(UNFPA), Dr. Natalia Kanem akizungumza kwenye maadhimisho ya hayo.
”
Takwimu zilizotokana na utafiti uliofanywa mwaka 2014 na Ofisi ya Taifa
ya Takwimu ( NBS) juu ya Watu wenye Uwezo wa Kufanya Kazi zimeonyesha
kuwa asilimia 43.8 ya watoto wa kike hushiriki katika shughuli za
nyumbani zisizo za kiuchumi na kiwango cha wasichana walioajiriwa ni
asilimia 47.5 wakati wavulana ni asilimia 52.5 hivyo, tuna kila sababu
ya kumkomboa mtoto wa kike”, Amesema Mhe. Ummy.
Amesisitiza
kuwa silaha kubwa ya kumkomboa mtoto wa kike ni kumpa elimu bora na ya
kutosha pia kupinga mila na tamaduni potofu juu ya watoto hao kwakua
ndizo zinazoleta changamoto nyingi zikiwemo za ndoa na mimba za utotoni
pamoja na fursa ndogo za kupata elimu na ajira.
Aidha,waziri
huyo ametoa wito kwa Watendaji wa Serikali ngazi ya Mikoa na
Halmashauri kuhakikisha wanaendelea kutoa elimu kwa jamii juu ya
kumlinda mtoto wa kike na kuwekeza katika maendeleo yake pia waendelee
kuelimisha umma kuhusu mabadiliko ya Sheria ya Elimu inayotoa katazo la
kuoa au kuolewa kwa watoto wenye umri chini ya miaka 19.
Amelipongeza
Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya Watu Duniani
(UNFPA) kwa jitihada zao za kuwajengea wasichana uwezo wa kujitambua na
kufahamu masuala mbalimbali ya kijamii yanayoendelea pia ametoa wito kwa
wadau kuangalia namna ya kuwafikia wasichana wengi waliopo maeneo ya
vijijini.
Imeandaliwa na Jacquiline Mrisho – MAELEZO
0 maoni:
Chapisha Maoni