Virusi vya hepatitis vinaua watu wengi zaidi ya Ukimwi na hata maradhi ya kifua kikuu, utafiti wa miaka 23 umebaini.
Kwa mujibu wa
utafiti huo uliochapishwa katika jarida la Lancet, maambukizi ya virusi
vya hepatitis vilisababishavifo vya watu milioni moja u nusu mwaka wa
2013 licha ya kuweko kwa madawa na hata chanjo dhidi yake.
''Mwaka wa wa 2013 watu 1.45 walipoteza maisha yao kutokana na Hepatitis.''
kwa mujibu wa
takwimu iliyokusanywa na shirika la afya duniani WHO mwaka huo kulikuwa
na vifo vya watu milioni moja nukta mbili (1.2) kutokana na maradhi
yanayosababishwa na Ukimwi.
Aidha WHO
inasema kuwa wakati huohuo yaani mwaka wa 2014 kulikuwa na takriban vifo
1.5 milioni kutokana na ugonjwa wa kifua kikuu.
Kutokana na utafiti huuu sasa WHO imeanza kupanga mikakati ya kupigana na virusi hivyo vya Hepatitis.
Watafiti wanasema kuwa kuna haja ya dharura sasa kwa mipango hiyo ya WHO ya kukabiliana na virusi hivyo vya Hepatitis.
Virusi vya Hepatitis ni vingi na huambukizwa kwa njia nyingi na hivyo kugawanywa katika vitengo vitano yaani A, B, C, D, E.
Virusi vya Hepatitis A na E vinaambukizwa kupitia ka maji na vyakula vilivyoambukizwa.
Virusi vya
Hepatitis B na C ndivyo vinavyosababisha idadi kubwa zaidi ya vifo
kutokana na kuwa vinasababisha kudhohofika kwa maini na hata kusababisha
mgonjwa kuambukizwa saratani ya ini.
Wanasayansi walifanya utafiti huo katika mataifa 183 kuanzia mwaka wa 1990 hadi mwaka wa 2013.
Watafiti hao
kutoka vyuo vikuu vya Imperial College London na chuo kikuu cha
Washington waligundua kuwa idadi ya vifo vinavyosababishwa na virusi vya
Hepatitis vimeongezeka kwa asilimia 60% katika kipindi hicho.
''Ni ajabu
kuwa maradhi haya ambayo tuna madawa yake ndiyo yanayouwa zaidi haswa
katika maytaifa yenye utajiri mkubwa.'' alisema profesa mmoja wa chuo
cha Imperial College London Dr Graham Cooke.
0 maoni:
Chapisha Maoni