Mshambulizi
wa Wales na Real Madrid Gareth Bale amesema kuwa timu yao haijuti
kubanduliwa nje ya mchuano wa Euro2016 mikononi mwa Ureno katika mkumbo
wa nusu fainali.
Wales
wakiongozwa na mchezaji aliyegharimu kitita kikubwa zaidi duniani
walikuwa wanatazamia kupata ushindi wao wa kwanza mkubwa, lakini
wakaambulia kichapo cha 2-0 mjini Lyon.
''Tulijitolea
kufa na kupona uwanjani, na kila mmoja wetu alikuwa na nia ya
kufanikisha ndoto yetu lakini wapi,ilikuwa ni bahati mbaya tu''
Waziri mkuu wa Uingereza anayeondoka David Cameron aliwamiminia sifa kochokocho.
''Vijana wa
Wales walijitoa kimasomaso, na bila shaka wamesisimua hisia kali na
ushabiki miongoni wa watu wa jamhuri ya Wales na muungano wa Uingereza
kwa Jumla, tunajivunia ufanisi wao huko Ufaransa kwenye kipute cha
Euro2016.''
Waziri
wa kwanza wa Wales Carwyn Jones alisema ni huzuni kuwa safari yao
imefikia kikomo japo akakariri kuwa ilikuwa ni jambo la kujivunia kwa
Wales kutinga hatua hiyo ynusu fainali.
Hii ndio iliyokuwa mara ya kwanza kwa Wales kufuzu kwa hatu hiyo.
Awali Wales walifuzu kwa hatua ya robo fainali ya kombe la dunia mwaka wa 1958.
Baada ya kutoka sare tasa kufikia kipindi cha mapumziko Cristiano Ronaldo alifuma mkwaju w kichwa kimiani kunako dakika ya 50.
Dakika tatu tu baadaye mkwaju wake ulimgonga Nani na kuelekea kimiani kwa bao la pili.
0 maoni:
Chapisha Maoni