Jumatatu, 18 Julai 2016

UEFA yatoa orodha ya wachezaji wanaowania tuzo ya mchezaji bora wa mwaka, Neymar apigwa chini


Chama cha Soka barani Ulaya (UEFA) kimetangaza oodha ya wachezaji 10 ambao watawania tuzo ya mchezaji bora wa mwaka barani Ulaya.
Katika hali ambayo imewashangaza wengi, mshambuliaji wa Barcelona, Neymar amekosekana katika oodha hiyo licha ya kuisaidia Barcelona kushinda kombe la Liga kwa msimu wa 2015/2016 kwa kufunga goli 31 katika michezo 49.
Aidha katika orodha hiyo, hakuna mchezaji hata mmoja wa ambaye anacheza Ligi Kuu ya Uingereza hali ambayo inafanya kuwepo na mtizamo tofauti kuhusu ubora wa ligi hiyo.
Wachezaji ambao wametajwa ni Gareth Bale, Gianluigi Buffon, Antoine Griezmann, Toni Kroos, Thomas Muller, Manuel Neuer, Luis Suarez, Pepe, Cristiano Ronaldo na Lionel Messi.

0 maoni:

Chapisha Maoni