MBUNGE wa jimbo la Mufindi Kusini Mkoani Iringa
Mendrad Kigola amesema tatizo la uhaba
wa maji lililokuwa linazikabili shule za
msingi jimboni humo,linaendelea kutatuliwa
kwa kasi kubwa, ambapo kwa sasa amechimba visima 5 vyenye thamani ya Tsh.Mill.60 huku kila
kisima kimoja kikigharimu kiasi cha Tsh.Mill 12 katika shule za Msingi zilizopo
jimboni humo,ikiwa ni moja ya utekelezaji wa ahadi yake aliyoliyoitoa wakati wa
kapeni za uchaguzi mkuu 2015,kuwa endapo atapewa ridhaa ya kuwa mbunge atahakikisha shule za Msingi
zilizopo jimboni humo zinapata maji safi na salama.
Akizungumza jana katika kijiji cha Kinegembasi Kata ya Itandula wakati wa zoezi la uchimbaji kisima katika
shule ya msingi kinegembasi likiendelea Mbunge Kigola alisema lengo la kuchimba
visima hivyo katika shule za msingi ni kutaka kutatua kero ya ukosefu wa maji
safi na salama katika shuleni.Pia
alisema maji hayo yatawanufaisha wananfunzi na jamii inayowazunguka kwa ujumla.
‘’’’’’Baada ya kuona watoto
wa shule za msingi wanahangaika namana ya kupata maji safi na salama nikaona
nguvu zangu zielekee huko kuchimba visima,ambapo hadi sasa nimechimba visima
vitano katika shule za msingi zilizopo
jimboni kwangu.Shule hizo ni Wangamaganga ,Ihangana twa,Lugema, Ikaning’ombe ,Pamoja
na shule ya Msingi Kinegebasi ‘’’’’alisema Kigola
Kigola alisema jumla ya kata 16 zilizopo jimbo lai Mufindi
Kusini kati yake , kata 14 zinanufaika na maji safi na salama,ambapo asilimia
65 ya wananchi wananufaika na maji hayo, ingawa bado kata 2 zenye chanagamoto
ya uhaba wa maji kutokana na mazingira yake kuwa kame,ila anaendelea kupambana
na kuhakikisha anatatua tatizo hilo.
Aidha Kigola alisema kwa muda wa miezi 6 amechimba visima
12 kama mbunge kwa kushirikiana na wadau, amekarabati visima
43 viliyotokana na uchakavu.Pia alisema toka mwaka 2011 alipochaguliwa mpaka
mwaka 2016 amechimba visima 28 kwa nguvu zake yeye mwenyewe kama mbunge bila
mchango wa wananchi.ataendelea kupambana kuhakikisha kata ya Itandula na …..zenye
ukame zinafikiwa na maji ili wananchi waondokane na kero hiyo na hatimae waweze
kupata maji safi na salama
Alisema kwa bajeti ya
fedha 2016/17 serikali imetenga kiasi cha Tsh.1.56 Till.kwa ajili ya maji,na Halmashauri ya Mufindi imetengewa
kiasi cha Tsh.Bill 2.3,hivyo kwa kata mbili zilizobakia,zenye uhaba wa maji kutokana na
ukame atahakikisha ufumbuzi unafanyika kuondoa tatizo hilo.
Kwa upande wake Diwani wa kata ya Itandula Hezron Muyinga
alisema kuwa kitendo cha mbunge huyo kuangazia sekta ya maji ukizingatia maji ni muhimu sana katika Afya
ya binadamu.
Muyinga alisema kulikuwa na kero kubwa ya bupatikanaji wa maji katika shule za
msingi,ambapo walimu walikuwa na wananchi walikuwa wanatembea umbali wa zaidi
ya km 2 hadi 5 kutafuta maji ambayo hayakuwa safi na salama.Pia alisema wanamuunga
mkono mh.mbunge kwa kuona umuhimu wa kuwapatia wananchi wa wilaya yake maji
safi na salama
‘’’’Hapo awali maji
yalikuwa yanauzwa ndoo moja kwa kiasi
cha Tsh. 500 ,hii ilikuwa ni kero kubwa kwa wananchi kukosa usingizi ,pamoja na
walimu kupoteza muda wao mwingi kutafuta maji na kushindwa kutumia muda wao fundisha’’’’alisema
Muyinga.
0 maoni:
Chapisha Maoni