Alhamisi, 7 Julai 2016

CHAMA CHA MAPINDUZI CCM IRINGA KIMEJIPANGA KUKABILIANA NA VIJANA WATAOLETA VURUGU MKUTANO MKUU DODOMA

  Posted by Esta Malibiche July 7/6/2016  in | Comments : 

Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi ccm Iringa mjini Abeid Kiponza akizungumza na wandishi wa habari 





Chama cha Mapinduzi  ccm Iringa mjini kimejipanga kuhakikisha kinalinda mkutano mkuu wa ccm unaotarajiwa kufanyika tarehe 23/7/2016 mkoani Dodoma,kuwa unafanyika kwa  Amani na utulivu kama ilivyopangwa.
Akizungumza na wandishi wa Habari  katika ofisi za ccm wilaya ya Iringa ,Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Iringa Mjini Abed Kiponza   alisema nimesikitishwa  sana na kitendo cha baraza la vijana chadema Bavicha kutoa tamko la kutaka kuzuwia mkutano mkuu wa ccm usifanyike.
‘’’’’Natamka kwa niaba ya wanaccm Iringa Mjini,na tutakabilana na yeyote atakaeleta vurugu ama kuonyesha dalili za uvunjifu wa Amani.Tumejipanga na tuko tayari kupambana na wale wote wataoleta fujo za makusudi wakati mkutano mkuu ukiendelea hatutamvumilia. ‘’’’’alisema Kiponza.
 Kiponza alisema kuwa mkoa wa Iringa inaunga mkono juhudi zinazifanywa na Dr. john Magufuli kwa kuiletea heshima ccm na Tanzania kwa ujumla.
 Alisema wanaccm Iringa wanamuunga mkono kwa asilimia mia moja na hawatasita kumpigia kura za ndiyo mwenyekiti mpya wa chama hicho Taifa Dk John Magufuli ili aendelee kutekeleza yote yaliyoandikwa katika Ilani ya chama hicho kwa lengo la kukijenga chama  na serikali kwa ujumla
 Kiponza alisema kuwa Dk Magufuli ambaye ni rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM  kwa muda alioingia madarakani amefanya mambo mengi yanayoyafanya watanzania na hata watu walio nje ya nchi kukubaliana na utendaji wake.
 “Tunampongeza rais wetu mchapazi Dk John Magufuli kwa kazi kubwa anayoifanya kwa ajili ya maendeleo ya taifa letu,kazi anayoifanya siyo tu inamletea heshima yeye bali inaliletea heshima Taifa letu linaloaminiwa na kupendwa duniani”’’’alisema Kiponza
 “Tunamtaka Magufuli achukue chama na kuja kutekeleza yote anayoyafanya kwa lengo la kuimarisha chama chetu,pia tunampongeza mwenyekiti wetu anayetarajia kukabidhi chama Jakaya Kikwete kwa kuwa ametekeleza wajibu wake kwa kipindi cha miaka kumi na kuiacha nchi katika hali ya amani”’’’’alisema.
 Aidha Kiponza aliviomba vyombo vya ulinzi na usalama kuwa makini na kundi hilo ambalo linahatarisha Amani ya Nchi kuwachukulia hatua sitahiki ili taifa liendelee kubaki katika hali nya amani na utulivu.
Kwa upande wake mwenyekiti wa Jumuiya ya Vijana ya Chama cha Mapinduzi (UV CCM)Iringa Mjini Kaunda Mwaipyana alisema jumuiya ya vijana wilayani humo imejipanga kulinda mkutano huo na licha ya vitisho kutoka kwa vijana wa Chadema wanaondai watazuia mkutano huo.
 Kaunda alisema Uvccm Iringa Mjini wamepokea kwa masikitiko makubwa tamko la  baraza la vijana la Chadema lililotangaza kuzuia mkutano huo usifanyike na kuongeza kuwa  Uvccm wilayani humo wamejipanga kwenda Dodoma kuhakikisha ulinzi unaimarika na hawatamvumilia mtu yeyote atakaeleta vurugu  za makusudi katika eneo linalofanyika mkutano
 “Sisi vijana tumejipanga kuulinda mkutano huo tunaomba viongozi wetu wawe na amani kwani jukumu la ulinzi wa chama na mali za chama ni jukumu la UV CCM|”.alisema Mwaipyana.
 Joseph Mgongolwa  ni mlinzi wa  chama wilaya ya Iringa nae aliwashauri vijana wa Bavicha  waliojipanga kwenda Dodoma kuzuia mkutano huo kuacha mara moja kwa kuwa kitendo hicho kinaweza kuwasababishia matatizo  makubwa

Maoni 1 :