Waziri
Mkuu na Makamu wa kwanza wa Rais mstaafu Mzee John Samwel Malecela akiwa
ameongozana na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Jordan Rugimbana wakisalimiana na
Viongozi wa skimu ya Umwagiliaji ya zabibu iliyopo Chinangali II
Chamwino wakati walipotembelea skimu hiyo mwishoni mwa wiki.
Afisa
Kilimo Wilaya ya Chamwino Ndg. Godfrey Mnyamale akiwasilisha taarifa ya
mradi wa skimu ya Umwagiliaji wa zabibu ya Chinangali II kwa mkuu wa
Mkoa wa Dodoma Jordan Rugimbana na Mzee Malecela (hawapo pichani) wakati
walipotembelea skimu hiyo mwishoni mwa wiki. Wengine ni viongozi wa
skimu hiyo.
Waziri
Mkuu na Makamu wa kwanza wa Rais mstaafu Mzee John Samwel Malecela
akimweleza Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Jordan Rugimbana (kushoto) changamoto
zinazo didimiza kilimo cha Zabibu Dodoma na kumtaka kufanya kila awezalo
kufufua zao hilo sambamba na kuondoa tatizo la njaa Dodoma wakati
viongozi hao walipotembelea skimu ya Umwagiliaji wa zabibu ya Chinangali
II mwishoni mwa wiki.
Mkuu wa
Mkoa wa Dodoma Mhe. Jordan Rugimbana akiahidi kufufua zao la zabibu
Mkoani humo na kuondoa tatizo la njaa kwa kufufua skimu zote za
umwagiliaji zinazolegalega na kukosa uongozi imara wakati akizungumza na
viongozi wa skimu ya umwagiliaji wa Zao la zabibu iliyopo Chinangali II
Chamwino mwishoni mwa wiki.
Mkuu wa
Mkoa wa Dodoma Jodan Rugimbana na Waziri Mkuu na Makamu wa kwanza wa
Rais mstaafu Mzee John Samwel Malecela wakikagua mitambo ya kusukuma
maji kwenye skimu ya Umwagiliaji ya zabibu iliyopo Chinangali II
Chamwino wakati viongozi hao walipotembelea skimu hiyo mwishoni mwa
wiki, wengine ni viongozi wa skimu hiyo.(P.T)
0 maoni:
Chapisha Maoni