Waziri
wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi wa Tanzania Bara na Zanzibar wamekutana na
kufanya mkutano na watendaji wa Mamlaka ya Uvuvi wa Bahari Kuu katika
mkutano wa pamoja na watendaji wa Mamlaka hiyo, uliofanyika Fumba,
Zanzibar.
Katibu
Mkuu Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Zanzibar Juma Ali
Juma akiwakaribisha Mawaziri wanaoshughulikia Uvuvi wa Tanzania Bara na
Zanzibar katika Mkutano wa pamoja uliozungumzia mikakati ya kuimarisha
Uvuvi wa Bahari Kuu Tanzania uliofanyika Mamlaka ya Usimamizi wa Bahari
Kuu Zanzibar iliopo Kijiji cha Fumba, Wilaya ya Magharibi B.
Waziri
wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi wa Zanzibar Hamad Rashid Mohd
akizungumza na watendaji wa Mamlaka ya Uvuvi wa Bahari Kuu katika
mkutano wa pamoja uliofanyika Ofisi ya Mamlaka ya Usimamzi wa Bahari Kuu
iliyopo Fumba.
Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Uvuvi wa Bahari Kuu Rashid Bakari Hoza
akieleza shughuli zinazofanywa na Mamlaka hiyo katika Mkutano
uliowashirikisha Mawaziri wanaosimamia masuala ya Uvuvi wa Zanzibar na
Tanzania Bara.
Waziri
wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi Dkt. Charles Tizeba akisisitiza jambao kwa
watendaji wa Mamlaka ya Uvuvi wa Bahari Kuu katika mkutano wa pamoja na
watendaji wa Mamlaka hiyo, (kulia) Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo
na Uvuvi Hamad Rashid Mohd.
Picha na Makame Mshenga/Maelezo Zanzibar.
0 maoni:
Chapisha Maoni