Licha
ya kutinga katika hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika lakini
kwa upande mwingine kumekuwa na maumivu kwa Yanga baada ya Chama cha
Soka cha Afrika (CAF) kuikuta na makosa iliyoyafanya katika mchezo dhidi
ya Sagrad Esperanca ya Angola.
Kamati
ya Nidhamu ya CAF iliyofanya kikao chake makao makuu ya CAF yaliyopo
Cairo, Misri iliikuta Yanga na kosa la kumsonga refa wa mchezo huo
pamoja na kupoteza muda baada ya Esperanca kupiga penati na hivyo
kuipiga Yanga faini ya Dola 10,000 za Kimarekani.
Aidha
CAF imewapunguzia Yanga adhabu kwa kuitaka kulipa Dola 5,000 ambazo
zinakaribia kufika Milioni 12 kwa pesa ya Tanzania lakini kuwapa
masharti kuwa wasirudie kosa hilo.
Katika mchezo huo uliochezwa Mei, 18, Yanga iliibuka na ushindi wa goli 2-1.
Aidha
CAF imeipiga faini ya Dola 10,000 Mo Bejaia ya Algeria kwa kosa la
mashabiki wake wa hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho kurusha fataki
katika mchezo wake na Yanga, mchezo huo ulimalizika kwa Yanga kukubali kichapo cha goli moja kwa bila.
0 maoni:
Chapisha Maoni