Wasanii nchini wametakiwa kuchangamkia fursa ya kazi za sanaa ambayo inadhaminiwa na British Council Tanzania.
Wito
huo umetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Waziri wa Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye wakati wa Uzinduzi wa Fursa ya Sanaa
kwa Tanzania na Afrika Mashariki ambayo Mdhamini wake ni British Council
Tanzania.
Mhe.
Nnauye amesema kuwa, uzinduzi wa fursa hiyo utawasaidia wasanii nchini,
Mashirika mbalimbali yakiwemo Makampuni ya ndani ya Tanzania pamoja na
Afrika Mashariki pamoja na Uingereza.
Amesema
kuwa, fursa hiyo ni kubwa kwa wasanii nchini na kwa Taifa kwa ujumla,
hivyo ameipongeza British Council Tanzania kwa kuja na wazo hilo zuri
kwa manufaa ya wasanii nchini.
‘’Napenda
nichukue nafasi hii kuwapongeza British Council Tanzania kwa
kuwashirikisha wasanii na Makampuni mbalimbali na kuhakikisha kuwa fursa
hizi zinamfikia kila msanii ndani ya Tanzania na kuwawezesha
kushirikiana pamoja kwenye Sekta ya Sanaa na Utamaduni ndani ya Afrika
Mashariki na Uingereza kwa ujumla’’, alisema, Mhe. Nnauye.
Ameongeza
kuwa Serikali kupitia Wizara yake imekuwa ikishirikiana na wadau
mbalimbali ndani na nje ya Tanzania katika kuwawezesha wasanii katika
kukuza vipaji vyao na kupata fursa zinazowawezesha kuitangaza nchi yao.
‘’Serikali
inatambua changamoto zinazowakabili wasanii wetu na imejikita katika
kuhakikisha kuwa inatoa fursa zilizopo kwa wasanii wetu’’.
Mhe.
Nnauye amesema kuwa, Serikali itaendelea kuwa mstari wa mbele
kuhakikisha kwamba inazidi kushirikiana na British Council Tanzania na
wadau mbalimbali ili kukuza vipaji vya wasanii hao.
Kwa
upande wake Mkuu wa Masuala ya Sanaa Kenya na Afrika Mashariki toka
British Council, Bi. Rocca Gutteridge amesema kwamba, fursa
inayodhaminiwa na British Council inalenga kuwawezesha Wasanii wa
Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla kuwa karibu kwa kushirikiana
katika vipaji vyao na hivyo wameanzisha na platifomu maalum ambayo
wasanii hao watakuwa wakisaidiana katika kazi zao.
0 maoni:
Chapisha Maoni