Wabunge
wanawake kutoka UKAWA, wametoka bungeni kufuatia Mbunge wa wa Ulanga,
Mhe. Goodluck Mlinga kusema kuwa wabunge wa viti maalum kutoka UKAWA
wanapewa nafasi hizo kwa kuwa na mahusiano na viongozi wa juu wa vyama
vyao.
Baada
ya kutamka maneno hayo, mmoja wa wabunge wa viti maalum aliomba
mwongozo kutoka kwa Naibu Spika, Dkt. Tulia Ackson na alipoona kuwa
hapewi nafasi wabunge wanawake wa upinzani kwa pamoja walisimama na
kutoka nje ya ukumbi wa bunge.
Akizungumza
na waandishi wa habari baada ya kutoka nje ya bunge, Mbunge wa Kawe na
Mwenyekiti wa BAWACHA, Halima Mdee amesema wanaumia wao kama wabunge
wanawake kufanyiwa vitendo hivyo na spika akiwa ni mwanamke bila
kuchukua hatua yoyote.
Amesema
sababu ya kuomba mwongozo ilikuwa ni kumtaka, Mhe. Mlinga afute kauli
aliyoisema awali lakini hakuna hatua iliyochukuliwa na kwasababu spika
ameshindwa kuchukua hatua kwa pamoja wabunge wa UKAWA wanaandika barua
ya kujitoa Chama ca Wabunge Wanawake (TWPG).
“Tunajua
nchi hii bado ina mfumo dume lakini usifike hii na kila tukikutana
katika vikao vya Chama cha Wabunge Wanawake tunazungumza lakini hata leo
spika ni mwanamke lakini hajafanya kitu,
“Mhe.
Mlinga anasema wabunge wa viti maalum kutoka UKAWA wanaingia bungeni
mpaka wawe na mahusiano na viongozi na sisi tuna taratibu zetu kama
chama ili kumpitisha mbunge lakini kama ni hivyo hata wao wabunge wao
wanalala na viongozi wao ndiyo wanawapa nafasi,” alisema Mhe. Mdee na
kuongeza.
“Kwa
pamoja wabunge wanawake wa upinzani tumekubaliana kuandika barua
kujitoa TWPG na tuwaachie chama chao kiwe Chama cha Wabunge wa CCM”
0 maoni:
Chapisha Maoni