Siku ya Dunia ya Urithi wa Kiafrika ni siku muhimu sana.
Ni
fursa ya kusherehekea utajiri wenye thamani kuu wa urithi wa utamaduni
na asili ya Afrika. Huu ni wakati wa dunia kusimama na serikali,
wanajamii na jumuia mbalimbali ili kusaidia moja ya rasilimali yenye
thamani kuu zaidi katika bara hili. Urithi na kiutamaduni na asili wa
Afrika ni nguvu kubwa amani na pia ni kichocheo cha maendeleo na
uvumbuzi.
Msukumo
wa siku hii ya kimataifa, kama ilivyotangazwa na nchi wanachama wa
UNESCO mwezi Novemba 2015, ni kuongeza uelewa wa kimataifa wa urithi wa
Afrika na kuhamasisha ushirikiano mkubwa katika kuulinda urithi huu. Hii
inajumuisha kila mtendaji, kuanzia kwa watoto wa shule, vijana wa kike
na wa kiume na wadau wote, ikiwa ni pamoja na Mfuko wa Kimataifa wa
Urithi wa Afrika , ambao mwaka huu unaadhimisha mwaka wake wa kumi.
Katika
muongo uliopita, tumefanya maendeleo makubwa ya kuongeza idadi ya
maeneo ya Afrika kwenye orodha ya urithi wa Dunia, hii ikienda pamoja na
kuboresha uhifadhi na usimamizi, kupanua ushiriki wa jamii na kuongeza
faida kwa jamii. Hata hivyo, kati ya maeneo 129 ya kiutamaduni na asili
katika bara la Afrika yaliyoorodheshwa katika ya orodha ya urithi wa
dunia, kuna maenoo 17 yaliyopo pia kwenye orodha ya maeneo ya urithi wa
dunia yaliyomo hatarini. Hatari zinazotishia maeneo hayo ni nyingi,
ikiwa ni pamoja na vita, ugaidi, ujangili,ongezeko la joto duniani,
upanuzi wa miji, na utafutaji wa mafuta na madini, yote haya
yanayojitokeza wakati kukiwa na mabadiliko makubwa ya kiuchumi na
kijamii.
Kulinda
na kukuza urithi wa kiutamaduni na asili ya Afrika ni kitu kilicho
katika kiini cha kazi ya UNESCO ya kuendeleza heshima na maelewano, na
kulinda vyanzo vya uasili na ubunifu. Hii pia ni muhimu katika
kuendeleza Ajenda ya 2030 ya Maendeleo Endelevu – kulinda urithi
husaidia kutengeneza nafasi za kazi, kukuza usawa wa kijinsia, na
kuondoa umaskini. Hakuna haja ya kuchagua kati ya urithi na ukuaji, kati
ya mandhari nzuri na maisha ya heshima – tukiwa na ujuzi sahihi na
uwezo ulio bora tunaweza kutumia urithi wa kiutamaduni na asili
kutengeneza ya ajira nzuri, na hivyo hali njema ya utu na heshima. Kwa
kuhifadhi maliasili, mito na mbuga, tunaweza kuwa na vyanzo vya ajabu
mno vya nishati mbadala kwa wote. Hakika, hili ni jambo la jema
kulifanya na uamuzi ulio makini. Huu ni ujumbe wa UNESCO leo.
Hii ni muhimu kwa Afrika – kwa wanawake na wanaume duniani kote, na hasa kwa vijana
0 maoni:
Chapisha Maoni