Mkuu
wa Mkoa wa Singida, Mhandishi Mathew Mtigumwe, amtumbua jipu
(amsimamisha kazi) kwa muda usiojulikana Mkurugenzi Mtendaji wa
Halmashauri ya Wilaya ya Singida, Simion Mumbe kwa tuhuma ya kutoa
taarifa ya udanganyifu kuwa watumishi hewa 19 wa halmashauri hiyo
hawajaisababishia hasara serikali.
Akizungumza
jana kwenye ufunguzi wa kikao cha maendeleo cha mkoani hapa, Mkuu wa
Mkoa wa Singida, Mhandisi Mtigumwe, alimwagiza Katibu Tawala Mkoa wa
Singida, Dk. Angela Mageni Lutambi, kumwandikia Mumbee mara moja barua
ya kumsimamisha kazi kupisha uchuguzi zaidi.
Akifafanua,
alisema kuwa Mumbee katika taarifa yake ya watumishi hewa, alionyesha
kuwa na watumishi hewa 19, lakini akabainisha kuwa watumishi hao
hawajaisababishia hasara yoyote serikali.
“Nilipotuma
tume kufuatilia suala la watumishi hewa katika halmashauri ya wilaya ya
Singida, ilibaini kuwa watumishi hao hewa, wameisababishia serikali
hasara ya zaidi ya shilingi 125 milioni,” alisema na kuongeza.
“Kwa
jumla taarifa ya Mumbee ililenga kudanganya jambo ambalo ni baya sana
na si kubaliani nalo kabisa. Halmashauri ya wilaya ya Singida hivi sasa
mhasibu wake amefikishwa mahakamani akituhumiwa kujiingizia kwenye
akaunti yake ya benki mishahara 11 ya watumishi hewa, sasa itakuwaje
mkurugenzi aseme hakuna hasara iliyosababishwa na watumishi hewa”.
Mhandisi
Mtigumwe kwa masikitiko, alisema kuwa hana nafasi ya kufanya kazi na
watumishi aina ya Mumbee ambao wanatoa taarifa za udanganyifu huku
serikali ikiingia hasara kubwa.
“Wakuu
wa wilaya nawaombeni sana mnisaidie kupambana na watumishi wa umma
wenye tabia kama ya Mumbee ya kutoa taarifa za udanganyifu. Kwa njia
hiyo mtakuwa pia mnamsaidia rais wetu katika vita vya kupambana na
watumishi hewa,” alisema.
Mkuu
huyo wa mkoa, alipomaliza kufungua kikao hicho, Afisa Tawala Mkoa
alitoa nafasi kwa uongozi wa halmashauri ya wilaya ya Singida, kutoa
taarifa yake ya madawati katika shule zake.
Mumbee
ambaye alionyesha dhahiri kupigwa mbumbuwazi na agizo la kusimamishwa
kazi, alisimama ili aweze kuisoma taarifa hiyo ambayo alikuwa nayo.
Bila
shaka Mumbee aliamini kuwa atasimama kufanya kazi pale atakapopewa
barua ya kusimamishwa hivyo alisimama tayari kuanza kuisoma taarifa
hiyo.
Lakini
ghafla mkuu wa mkoa, aliingilia kati na kumwambia Mumbee kwamba kwa
wakati huo hakuwa mtumishi wa umma kwa vile amemsimamisha kazi.
Alimwagiza kazi ya kusoma taarifa hiyo amkabidhi mtumishi mwingne na
yeye aondoke kwenye mkutano huo.
Mumbee
kwa unyonge aliacha karatasi za taarifa hiyo juu ya meza na kuondoka
kwa miguu hatua zaidi ya mia mbili kurudi ofisini kwake kuchukua vilivyo
vyake. Wakati wa kwenda kwenye kikao hicho, Mumbee alikwenda na gari
lake la kazi.
Na Nathaniel Limu, Singida
Mkuu
wa mkoa wa Singida, Mhandisi Mathew John Mtigumwe,a kitangza rasmi
uamuzi wa kumtubua jipu (kumsimamisha kazi), Mkurugenzi Mtendaji wa
Halmashauri ya wilaya ya Singida, Simion Mumbee, kwa tuhuma ya kutoa
taarifa ya udanganyifu kuhusu watumishi hewa.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida, Simion Mumbee (mwenye
koti jeusi) akisikiliza kwa makini agizo lililokuwa linatolewa na Mkuu
wa Mkoa wa Singida, Mhandisi Mathew Mtigumwe la kumsimamisha kazi.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida, Simion Mumbee akijiandaa
kusoma taarifa yake ya madawati hata hivyo Mkuu wa Mkoa wa Singida,
Mhandisi Mathew Mtigumwe alimzuia kwa madai kuwa tayari alikuwa si
mtumishi tena wa umma.
Picha
ya juu na chini ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya
Singida, Simion Mumbee akirejea kwa miguu ofisini kwake baada ya
kusimamishwa kazi na mkuu wa mkoa wa Singida, Mhandisi Mathew Mtigumwe.
(Picha na Nathaniel Limu)
0 maoni:
Chapisha Maoni