Jumapili, 15 Mei 2016

ELISHA MWAMPASHI AWATAKA WATANZANIA KUIFANYIA KAZI KWA VITENDO KAULI YA MH.RAIS YA HAPA KAZI TU



Kaimu katibu wa chama cha mapinduzi ccm mkoa wa Iringa  ambae pia ni katibu wa ccm Iringa Mjini mkoani hapa, Elisha Mwampashi amewataka  amewataka watanzania kuunga mkono juhudi zinazofanywa na serikali ya awamu ya tano kwa vitendo ili Taifa liweze kupiga hatua kimaendeleo
Akizungumza leo[jana]na wananchi jamii ya wafugaji ambao ni wamasai  wakati akifungua shina la kijiwe cha wakeleketwa ccm katika kitongoji cha Mahove kata ya mauninga jimbo la Isimani Halmashauri ya Iringa  kilichojengwa  na wamasai kwa lengo la kuunga mkono kazi mbalimbali zinazfanywa na mh. Rais dkt Magufuli na serikali yake.
Mwampashi alisema  kauli mbiu iliyoandikwa katika kijiwe hicho ya Hapa kazi  tu inatakiwa kuungwa mkono kwa vitendo  kwa kufanya kazi kwa bidii kila mmoja na nafasi yake mahali alipo,na kwa wafugaji wafuge kwa wingi pamoja na wakulima nao walime kwa bidii ili kuwa na ziada ya chakula hapo ndipo tuataitendea haki kauli hiyo
‘’’’’’’Lengo la kijiwe hiki na kauli yake ni kuunga mkono juhudi za mh.Rais kwa kazi anazofanya.Tutumienafasi hii kuona namna ya kujikwamua kiuchumi ili kitongoji cha mahove kipige hatua kimaendeleo ,wakulima mlime na wafugaji mfuge kwa kuzingatia kanuni na taratibu za ufugaji kwa kfanya hivyo tutakuwa tumeitendea haki kauli ya hapa kazi tu’’’’alisema
Baada ya uzinduzi wa shina la wakeleketwa ulifanyika mkutano wa hadhara ambapo wananchi walitoa kero zao kuhusiana na chanagamoto zinazowakabili ambazo hazijatatuliwa kwa muda mrefu  hadi sasa na hatiamae  kutojua muafaka wa hitaji lao
Mzee  Klelu Mahiteni alisema kuwa kutokana na uwingi wao pamoja na vigezo vilivypo waliiomba serikali kuwapatia  kijiji  ili waweze kupata huduma kama wananchi wengine lakini jambo la kushangaza hadi hivi sasa hakuna kinachoendelea ukizingatia katika kampeni za uchaguzi mkuu 2015 aliyekuwa mgombea wa ubunge kupitia chama cha mapinduzi mh.Willium Lukuvi ambae ni waziri wa ardhi na makazi na mbunge wa jimbo hilo aliwaahidi kuwa endapo atapewa dhamana ya ubunge atatoa upendeleo wa kupewa kijiji .
Tulikaa na uongozi wa serikali za mitaa tukaandika barua ya kukumbusha ombi letu la kupewa kijijiu lakini inashangazwa kuona barua hiyo haifanyiwi kazi wala kurudisha majibu kama imekubalika au kukataliwa,tunaomba mh.mbunge wetu atusaidie kwa kusimamia kama alivyoahidi kipindi cha kampeni ya uchaguzi mkuu wakati akiomba kura’’’’alisema
Wakizungumza katika mkutano huo wananchi walisema changamoto nyingine zinazowakabili nipamoja na kivuko, darasa la chekechea ili watoto waweze kusoma maeneo jirani na makazi yao,Zahanati ,bati kwa ajili ya kuezeka nyumba ya mchungaji wa kanisa la kkt ambazo mh.Mbunge Lukuvi aliahidi kutoa.
Alisema anaiomba serikali iweze kuwafikilia ili waweze kuepukanan na adha ya kushindwa kuendelea na shughuli zao,kutokana na mvua kunyesha hasa katika kupata matibabu  pamoja na watoto kushindwa kwenda shule kutokana na maji kujaa wakati wa masika.
Tatizo hili limedumu kwa muda mrefu,na serikali inajua hilo lakini tunaona wapo kimya tu bila kulifanyia kazi .Mvua zikianza kunyesha hali ya usalama inakuwa hatiani na watoto wanashindwa kwenda shule pamoja ’’’alisema
Alisema serikali inatakiwa kusimamia  kuweka  mgogolo baina ya wakulima na wafugaji na kuweka utaratibu ambao utasaidia makundi haya yasiingilianae na  kusababisha mtafaruku utakao vuruga amani katika jamii miongoni mwao kutokana na wafugaji  kupitisha mifugo yao katika vyanzo vya maji,na mashambani na hatimae kusababisha maji kukauka.



0 maoni:

Chapisha Maoni