Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa amemtaka
mkandarasi wa Kampuni ya Estim Construction anayejenga Daraja la Ruvu
Chini linalounganisha barabara ya Bagamoyo-Msata yenye urefu wa Km 64
mkoani Pwani kukamilisha ujenzi wa daraja hilo ifikapo mwezi Novemba
mwaka huu.
Prof.
Mbarawa amesema hayo wakati alipokagua ujenzi wa Daraja hilo na
kuhimiza kukamilika kwa wakati uliopangwa ili kuhakikisha barabara hiyo
inapitika majira yote ya mwaka na kurahisisha huduma ya usafiri kwa
wakazi wa mkoa wa Pwani na mikoa jirani.
“Hakikisheni
ujenzi wa Daraja hili unakamilika kwa wakati ili lianze kutumiwa na
wananchi kwa wakati wote kwa ajili ya kujiletea maendeleo yao binafsi,”
alisema Prof.Mbarawa.
Vile
vile Profesa Mbarawa amemhimiza Mkandarasi huyo kuzingatia viwango vya
ubora kulingana na thamani ya fedha ili Daraja hilo liweze kudumu kwa
muda mrefu.
“Ni
vema daraja hili lijengwe kwa ubora unaotakiwa kulingana na thamani ya
fedha ili liweze kuhimili athari za Mvua zinajitokeza eneo hili,”
alisisitiza Waziri Mbarawa.
Aidha
Waziri Mbarawa ameongeza kuwa Serikali inaendelea kufanya upembuzi
yakinifu na usanifu wa kina katika miradi inayotarajiwa kuanza
kutekelezwa maeneo mbalimbali nchini.
Zaidi
ya Shilingi Bilioni 129zitatumika katika ujenzi wa Barabara ya
Msata-Bagamoyo Km 64, Daraja la Ruvu chini yenye urefu wa Mita 140
pamoja na Barabara ya Maingiliano ya Daraja hilo yenye urefu KM 4.2.
0 maoni:
Chapisha Maoni