Mkuu
wa mkoa wa Singida, mhandisi Mathew Mtigumwe (kulia), akimwapisha Mkuu
wa wilaya ya Ikungi Miraji Mtaturu. Hafla hiyo imefanyika kwenye ukumbi
wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa mkoa mjini Singida.Picha na Nathaniel
Limu.
MKUU
mpya wa wilaya ya Ikungi mkoani Singida, Miraji Mtafuru, amesema
kipaumbele chake cha kwanza katika kuwatumikia wananchi, ni kuhakikisha
wananchi wote wanaondokana na dhana potofu kwamba serikali pekee ndiyo
yenye jukumu la kuiletea wilaya hiyo maendeleo.
Amesisitiza
kwamba dhana hiyo yenye lengo la kudumaza dhana maendeleo ya wilaya
hiyo changa,itafika wakati itabaki kuwa ni historia.
Wananchi wote watabadilika na kuwa na fikra sahihi kwamba maendeleo ya kweli ya wilaya ya Ikungi, yataletwa na wao wenyewe.
DC
Mtaturu ameyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari muda
mfupi baada ya kuapishwa na Mkuu wa mkoa mhandisi Mathew Mtigumwe
kwenda kuongoza wilaya hiyo pekee mkoani Singida, iliyopo mikononi mwa
Chama cha Upinzani (CHADEMA).
“Hatutakubali
mtu yeyote au kiongozi yeyote atumie elimu yake kudumaza maendeleo ya
wilaya ya Ikungi. Popote duniani, wananchi ndio wanaochangia kwa hali na
mali maendeleo yao. Dhana hii potofu kwamba serikali pekee ndio yenye
jukumu la kuiletea maendeleo ya wilaya ya Ikungi, tutaipiga vita kwa
nguvu zetu zote”,alifafanua zaidi.
Aidha,
amesisitiza kwamba atahakikisha wananchi wa wilaya hiyo changa ya
Ikungi hawatumiki vibaya na wanasiasa au mtu mwingine ye yote mwenye
lengo la upoteshaji.
Katika
hatua nyingine, Mtaturu alisema atasimamia kikamilifu elimu bora
itakayokidhi mahitaji ya karne hii inatolewa, ili wilaya hiyo iendelee
kupata vijana wengi wasomi ambao baadaye wataziendeleza familia zao
kiuchumi na kijamii.
“Tukiwa
na vijana wengi wasomi, wakulima wa wilaya yetu watalima na kufuga
kitaalamu na hivyo shughuli hizo zitakuwa na tija zaidi. Kwa ujumla
wasomi ndio watakaosaidia wilaya ya Ikungi kupaa kimaendeleo na
ikiwezekana ipite wilaya kongwe”,alisema kwa kujiamini.
Hata
hivyo,alisema hayo yote pamoja na maendeleo ya sekta zingine muhimu,
yatafanikiwa kwa kiwango kikubwa kwa vile atashirikisha watendaji wote
wa ngazi mbalimbali na wapenda maendeleo wa wilaya hiyo.
Wakati
huo huo,Mtaturu ametumia fursa hiyo kumshukuru rais Dk. Magufuli kwa
kitendo chake cha kumwamini na kumteua kama mkuu wa wilaya ya Ikungi,na
kuahidi kwamba hatamwangusha.
Imeandikwa na Nathaniel Limu
0 maoni:
Chapisha Maoni