Meneja anayeshughulika na masuala ya Mazingira wa kampuni ya vinywaji ya SABMiller  kanda ya Afrika, Bw.Muzi Chonco, ambaye yuko nchini kwa ziara ya kikazi mwishoni mwa wiki alifanya ziara katika Wizara ya Maji na Umwagiliaji ambapo alikukutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Mhandisi Mbogo Futakamba.
Bw.Chonco katika mazungumzo hayo aliweza kumweleza Katibu Mkuu  miongozo na  mikakati mbalimbali ya kampuni hiyo kuhusiana na utunzaji wa mazingira,matumizi sahihi ya maji ,utunzaji wa vya maji na miradi ambayo kampuni inasaidia kuendesha.
Kampuni ya SABMiller  kwa hapa nchini inamiliki kampuni ya kutengeneza vinywaji ya TBL Group ambayo inamiliki viwanda  mbalimbali vya kutengeneza vinywaji hapa nchini.
Katika ziara hiyo ya kikazi Bw.Chonco aliongozana na Meneja wa kiwanda cha kutengeneza bia cha TBL kilichopo Ilala jijini Dar es Salaam,Bw.Calvin Martin na maofisa wengine wa kampuni ya TBL Group.
Meneja mazingira wa SABMiller, Muzi Chonco
Katibu Mkuu Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Mbogo Futakamba ( kulia) akimsikiliza kwa makini  Meneja mazingira wa SABMiller, Muzi Chonco, wakati alipofanya ziara ya kikazi ofisini kwake Ubungo jijini Dar es Salaam, (Kushoto) ni Meneja wa  kiwanda cha bia cha TBL Group Ilala Dar es Salaam Bw. Calvin Martin.
Katibu Mkuu Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Mbogo Futakamba
mfutakamba 5
Katibu Mkuu Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Mbogo Futakamba (wa pili kutokea kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Meneja Mazingira wa SABMiller na Maofisa wa TBL Group walipomtembelea ofisini kwake mwishoni mwa wiki iliyopita