Jumatatu, 16 Mei 2016

BALAZA LA KIISLAMU IRINGA MJINI[BAKWATA] WAKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO




Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela amewataka viongozi wa dini ya kiislamu nchini kuishi kwa kufuata maadili ya kiislamu kama Qur’an tukufu inavyosema ili  waweze kuwaongoza waumini wao .
Akizungumza  na viongozi wa Balaza la waislamu Iringa Mjini katika wakati akifungua mkutano wa Bakwata  uliofanyika jana mkoani hapa  na kuhudhuriwa na wajumbe wa mbalimbali,Kasesela alisema  kiongozi  anatakiwa awe mcha mungu,muadilifu,mkweli,mwenye huruma kwa waumini wake,mkweli na asiyethubutu kujilimbikizia mali kwa kutumia wajibu au cheo cha uongozi alichonancho kwa manufaa yake binafsi.
Kasesela aliitoa kauli hiyo kufuatiwa kujiondoa kwa baadhi ya viongozi wawili ya bakwata Iringa mjini na  kushinikiza kufanyika uchaguzi upya, ambao ulitakiwa ufanyike jana jumapili kwa madai yao binafsi kuwa uongozi wa bakawata uliopo si halali,ndipo jeshi la polisi lilitupilia mbali omb hilo na kusitisha kuwepo kwa uchaguzi huo ambao ni batili hadi taarifa itakapotoka bakwata Taifa
Alisema kiongozi anatakiwa daima kuwa  mtumishi wa wale waliomuweka katika uongozi,kwa kuwa mnyenyekevu,mwenye kuwahurumia wale anaowaongoza na mwenye kuwapendelea analolipendelea katika nafsi yake
Alisema kipimo cha kiongozi mzuri ni uadilifu,kiongozi mzuri akiwa muadilifu huwa khalifa wa Alla[s.s] na akiwa si muadilifu huwa khalifa wa shetani,hivyo kwa kuwa uadilifu unasisitizwa katika Qur’an inapaswa jamii na waislamu kwa ujumla kuzingatia agizo hilo kwa vitendo.

0 maoni:

Chapisha Maoni