Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli
amewataka Wakurugenzi Watendaji wa Halmshauri zote nchini kuondoa kero
za wananchi na si kuwaongezea kero.
Hayo ameyasema leo kwenye hafla ya Kiapo cha Uadilifu wa Utumishi wa umma iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam.
“Anzisheni
miradi inayotatua kero za wananchi na si kuwaongezea kero, kila eneo
lina kero zake hivyo jitahidini kuziondoa,”alisema Rais Magufuli.
Amewataka
Wakurugenzi hao kufanya kazi kwa bidii kwa ajili ya wananchi kwani
wamechoshwa na kero hasa kwenye ushuru na kodi zisizo za lazima,
akitolea mfano mkulima wa mchicha na mpunga kutozwa kodi wakati amelima
kwa ajili ya chakula chake ya kwamba hili jambo halikubaliki.
Rais
Magufuli amewaambia Wakurugenzi kuwa anawaamini kwani uteuzi wao
ulifanywa kwa umakini na akaonyeshwa kushangazwa na waliokuwa wakibeza
uteuzi huo hasa waliosema kuwa amemteua mwenye cheti cha usimamizi wa
hoteli.
“Majina
kufanana si tatizo, mimi niliyemteu ni Bwana Luhende ambaye ana diploma
na masters (shada ya uzamili), Bwana Luhende hebu simama wakuone na
vyeti vyako,” alisema Rais Magufuli.
Aidha,
Rais Magufuli amesema kuwa hakubahatisha katika kuteua Wakurugenzi hao
na kuongeza kuwa kazi hiyo ameifanya kwa umakini mkubwa.
Rais
amewataka Wakurugenzi kuhakikisha wanakusanya na kusimamia kodi za
wananchi ili kuwaletea maendeleo na kuwaondolea matatizo ambayo
yamewachosha.
Kwa
upande wake, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano, Samia Suluhu Hassan
amewataka Wakurugenzi kuwa watumishi wa watu na si watawala.
Amewaasa
Watendaji hao kujifunza sheria na kanuni zinazohusiana na kazi zao na
kuwataka wawe waadilifu na wachapakazi ili kuwaletea wananchi maendeleo.
Naye Waziri Mkuu wa Tanzania, Mhe. Kassim Majali Majaliwa amewataka Wakurugenzi kuwa wawajibikaji, waadilifu na waaminifu.
“Ninyi
ni injini ya maendeleo katika nchi kupitia kwenye Halmashauri zenu na
kazi yenu kubwa ni kusimamia watumishi katika kuleta maendeleo katika
sehemu zenu,”alisema Majaliwa.
Amewataka
Wakurugenzi kukusanya kodi na kuzitumia katika miradi ya maendeleo kwa
uaminifu na kuwasisistiza kuzingatia thamani ya fedha katika mradi
husika (Value for Money)
Jumla
ya Wakurugenzi 185 wamekula kiapo cha uadilifu katika utumishi wa umma
na kuhudhuria mafunzo ya maadili yaliyoandaliwa na Ofisi ya Rais
Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma.
0 maoni:
Chapisha Maoni