Ijumaa, 1 Julai 2016

TANZANIA YAWA MWENYEJI WA MKUTANO WA KIMATAIFA WA MASUALA YA USALAMA WA MTANDAO WA TEKNOLOJIA

index
Na Mahmoud Ahmad Arusha
CHAMA Cha wakulima nchini TASO ,kanda ya ksikazini kimepiga marufuku mabanda ya maonyesho ya wakulima Nane nane yaliyopo  viwanja vya maonyesho vya Taso Themi Hill,jijini Arusha,kugeuzwa matumizi na kuwa ni ya biashara ya mama lishe na shughuli za ufugaji na kutaka yabakie kwa ajili ya maonyesho tu.
 
Hayo yamefikiwa jana kwenye awamu ya pili ya kikao cha uongozi wa Taso na wadau ambao ni wamiliki wa mabanda kilichohusu  maandalizi yamaonyesho ya wakulima Nane nane mwaka huu na kusisitiza kuwa Taso haifanyi biashara na hairuhusu wamiliki wa mabanda hayo kuyageuza na kuwa ni sehemu ya biashara.
 
Mwenyekiti wa Taso, Ather Kitonga, amesema iwapo Taso itaruhusu mabanda hayo kubadilishwa matumizi badala ya shughuli za maonyesho yakatumika kwa ajili ya biashara ,yatakuwa yamepoteza maana halisi ya mabanda ya maonyesho na Taso haiko tayari kwa hilo.
 
Amesema shughuli ya biashara zinafanywa na walinzi  kwa ajili ya kujiongezea vipato mara tu maonyesho ya wakulima yanapomalizika  na hiyo inatokana na mawasiliano duni kati ya halmashauri za wilaya  kupitia kwa maafisa kilimo na mifugo ambao huwa hawatembelei mabanda hayo mara maonyesho yanapomalizika.
 
Kitonga, amesema kupitia uduni huo wa mawasiliano walinzi wameyageuza mabanda hayo kuwa ni ya mama lishe, na ufugaji  na hivyo kwenda kinyume na malengo ya viwanja vya maonyesho ya wakulima.
 
Amesema kuanzia Juni 28 mwaka 2016 ni marufuku kwa halmashauri za wilaya kugeuza nyumba na mabanda yaliyoko ndani ya viwanja hivyo kuwa ni makazi ya kudumu na kuyageuza kuwa ni sehemu ya kufugia mbwa na kuku.
 
Kitonga, amesema Taso imezitaka halmashauri zote za wilaya ,kuhakikisha zinaondoa mbwa na kuku wanaofugwa kwenye mabanda hayo sanjari na kuhakiki walinzi wao na nyumba na mabanda ya maonyesho ili kudhibiti ubadilishaji wa matumizi kwa kuyageuza kuwa ni ya kufugia mifgo na wanyama .
 
.Aidha Taso imezitaka halmashauri zote za wilaya kuhakikisha zinakuwa na takwimu za teknolojia ya kilimo na mifugo ili kuwasaidia wananchi  kubadilisha shughuli zao na kuzifanya ziwe na tija badala ya kufanya kwa mazoea.
 
Kitonga, amesema ili teknolojia hizo ziwafikie walengwa lazima wataalamu wa kilimo waoteshe mbegu za vipando na  halmashauri zijikite kwenye  vipando kwa kutoa elimu kwa wakulima namna ya kulima kibiashara ili wapate faida .
 
Ameongeza kuwa Taso imejipanga kuhakikisha teknolojia ya kilimo inawafikia wakulima na maonyesho hayo yanakuwa ni yenye tija  na sio kuwa ya mazoea .
 
Amesema maonyesho hayo yanaanza rasm I Augosti mosi na kumalizika Augositi kumi na kuwataka  watakaoshiriki kwenye maonyesho hayo mwaka huu kuzingatia kalenda hiyo ambayo inakusudia kutoa muda mrefu zaidi kwa waonyeshaji badala ya kumalizika Augoti 8sasa kilele chake kitakuwa Augosti 10.
 
Kwa upande wake Katibu mkuu wa Taso kanda ya kasikazini Jeremiah Sembose, amesema  changamoto kubwa iliyopo ni kwenye vipando ambapo asimia 90% ya mbegu  hazina ubora  na hivyo vipando vinashindwa kutoa ujumbe halisi wa shamba darasa kwa wakulima wanaotembelea ili kujifunza.
 
Sembose, amesema kuwa tayari Taso, imeshapokea kauli mbiu ya maonyesho ya mwaka huu kutoka wizara ya kilimo isemayo Kilimo, uvuvi na mifugo ni nguzo ya maendeleo vijana shiriki kikamilifu hapa kazi tu.
 
Kuhusu maandalizi ya mabanda ya maonyesho, Sembose, amsema uongozi wa Taso, mara baada ya kutembelea  mabanda hayo haujaridhishwa na hatua ya maandalizi  na  imegundua kuna changamoto  mbalimbali .
 
Amezitaja baadhi ya changamoto hizo kuwa ni pamoja na kutokufikia asilimia 50%,maandalizi kwa halmashauri za wilaya za Same,Moshi  na Ngorongoro zikiongoza kwa kuwa na hali mbaya   ya maandalizi.
 
Sembose, amesema kutokana na hali hiyo, Taso, imezitaka halmashauri zote za mikoa ya Arusha, Manyara na Kilimanjaro,  kuhakikisha zinaanza maandalizi ambayo yatahusisha upakaji rangi mabanda yote, usafi, upandaji wa vipando ikiwa ni shamba darasa ,kuimarisha miundo mbinu, kubosha mazingira .

0 maoni:

Chapisha Maoni