Jumapili, 1 Mei 2016

MAMBO USIYOYAJUA KUHUSIANA NA UFOs (Unidentified Flying Objects)

bbb
 Na Benedict Liwenga (Maelezo)
…………………………………….
 
Katika Dunia tuishiyo sasa binadamu hatuko peke yetu, lakini tumejijengea dhana kuwa tunaishi peke yetu huku tukisahau kuwa Mungu kaumba viumbe kadha wa kadha vinavyoonekana na visivyoonekana.
Unaweza kushangaa ama kudhani kuwa namaanisha juu ya uwepo wa nguvu za kigiza, La Hasha!, mtu anapokuuliza kwamba Je unafahamu maana ya neno ‘UFO’ (Unidentified Flying Object)? Bila shaka watu wengi watakuwa hawafahamu kuhusiana na vitu hivi na wengine wanaweza kukupa maana nyingine tofauti na mada.
Neno UFO limechukua kasi kwenye vyombo vya habari vingi duniani hasa vya wenzetu wa nchi za Magharibi, pia upande wa Asia ambapo baadhi ya Wataalam wamajaribu kufuatilia kwa karibu juu ya vitu hivi na wapi vimetokea na madhumuni ya kuonekana ovyo katika maeneo tofauti na madhara yake lakini hakuna maelezo mazuri yanayoweza kuelezeka katika hilo, na hii imepelekea wataalam hao kuziita baadhi ya tafiti zao kuwa ni zisizoelezeka (Unexplained files about UFOs)
Ebu tujiulize maswali UFOs ni vitu gani, na malengo yake kuonekana duniani ni nini haswa?
UFOs ni Vyombo vyenye ukubwa tofauti na maumbile tofauti ambapo vingine vinakadiliwa kuwa na ukubwa wa futi 100 ama zaidi vingine na muonekano wake ni wa duara kama sahani kubwa la chuma lenye kung’aa (steel shaped-saucer), lakini pia vinaweza kuwa na umbo mengine tofauti kama vile maumbile ya pembe tatu ambapo kwa chini zinakuwa ya na taa zenye kutoa miale mikali ya mwanga yenye rangi ya bluu, nyekundu na nyeupe.
Continue reading →

0 maoni:

Chapisha Maoni