Jumanne, 10 Mei 2016

KAMISHNA MSAIDIZI KITENGO CHA HAKI ZA MTOTO AFUNGUA NYUMBA ZA KUNDI LA WATOTO


Kaimu Kamishna msaidizi kitengo cha haki za mtoto na marekebisho ya tabia, Steven Gumbo akikata utepe kuashiria ufunguzi rasmi wa mradi wa nyumba za kundi la watoto wanaoelekea ujanani katika kituo cha kulelea watoto cha Aman Center kilichopo mjini Moshi.
Jengo jipya lililojengwa kwa ufadhili wa Emirates National Bank of Dubai (ENBD) kwa ajili ya watoto wanaoelekea ujanani katika kituo cha kulelea watoto cha Aman Center kilichopo mjini Moshi.
Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha kulelea watoto cha Aman Center Meindert Schaap akimuonesha Kaimu Kamishna msaidizi kitengo cha haki za mtoto na marekebisho ya tabia, Steven Gumbo maeneo mbalimbali ya jengo hilo katika ramani.
Moja ya muonekano wa chumba katika jengo hilo.
Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha kulelea watoto cha Aman Center Meindert Schaap akizungumza wakati wa hafla ya ufunguzi rasmi wa jengo hilo.
Baadhi ya walimu na walezi wa watoto katika kituo cha kulelea watoto cha Aman Center wakifuatilia shughuli mbalimbali katika hafla hiyo.
Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha kulelea watoto cha Aman Center Meindert Schaap akiteta jambo na Kaimu Kamishna kitengo cha haki za mtoto na marekebisho ya tabia, Steven Gumbo wakati wa hafla ya ufunguzi wa jengo hilo.
Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha kulelea watoto cha Aman Center Meindert Schaap akimkaribisha Afisa Ustawi wa Jamii wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi ,Agnes Urassa katika Hafla hiyo.
Baadhi ya watoto wanaolelewa katika kituo cha Aman Center kilichopo mjini Moshi.

0 maoni:

Chapisha Maoni