Kila Juni 16 ya mwaka Bara la Afrika linaadhimisha sikiu ya mtoto wa Afrika, tunapoadhimisha kumbukumbu ya siku ya mtoto wa Afrika ambapo pia kwa mwaka huu 2016 ikiwa ni mara ya 26 tangu uliokuwa Umoja wa Nchi Huru za Afrika (OAU) uizindue siku hiyo mwaka 1991,
kwa kuona umuhimu wa siku hii, Taasisi ya Miradi na Maendeleo ya Miundombinu iliyo chini ya Wizara ya Fedha (UTT-PID) imeweza kushirikii tukio hilo pamoja na kucchangia kiasi cha fedha.
Katika ushiriki huo, Mkuu wa kitengo cha Mahusiano ya Umma na masoko UTT-PID, Bi. Eugenia Simon alieleza kuwa UTT-PID kwa kuona umuhimu wa siku ya Mtoto wa Afrika wameonelea kuchangia siku hiyo kwani ni faraja kwa watoto wote.
Aidha, Bi. Eugenia aliweza kutoa mfano wa Hundi  kwa watendaji wa mji mdogo wa Chalinze kwa ajili ya kuchangia maendeleo ya watoto wa mji huo.
UTT-PID pia inaendesha miradi yake ya viwanja katika Mkoa huo wa Pwani ikiwemo mji wa Chalinze na Bagamoyo. Ambapo katika mji huo wa Chalinze, UTT-PID ina mradi wa upimaji na uuzaji wa viwanja ujulikanao kama New Chalinze City huku ule wa Bagamoyo ukijulikana kama New Mapinga City.
WhatsApp-Image-20160617 (7)Mkuu wa kitengo cha Mahusiano ya Umma na masoko UTT-PID, Bi. Eugenia Simon (wa kwanza kulia) akifuatilia maadhimisho hayo ya siku ya mtoto wa Afrika katika mji wa Chalinze jana Juni 16.2016
WhatsApp-Image-20160617 (1)Mkuu wa kitengo cha Mahusiano ya Umma na masoko UTT-PID, Bi. Eugenia Simon akitembezwa katika moja ya mabanda yaliyokuwa yakionyesha bidhaa katika siku hiyo.
WhatsApp-Image-20160617Maadhimisho hayo yakiendelea.
WhatsApp-Image-20160617 (4)Mkuu wa kitengo cha Mahusiano ya Umma na masoko UTT-PID, Bi. Eugenia Simon akielezea maneno machache namna ya taasisi hiyo inavyofanya shughuli zake hapa nchini
WhatsApp-Image-20160617 (6)Mkuu wa kitengo cha Mahusiano ya Umma na masoko UTT-PID, Bi. Eugenia Simon akikabidhi hundi ya fedha kwa Mtendaji wa Chalinze kwa ajili ya watoto wa mji huo. (Picha zote na UTT-PID).