Alhamisi, 23 Juni 2016

SHIRIKA LA I,H,H INSANI YARDIM VAKFI KWA KUSHIRIANA NA JUMUIYA YA MUZDALIFA ZANZIBAR YATOA MSAADA WA FEDHA KWA MAYATIMA ZANZIBAR

va1Wafanya kazi wa Jumuia ya Muzdalifat wakitayarisha malipo ya Msaada kwa ajili ya Watoto Mayatima wanaosaidiwa na Shirika la Misaada la I,H,H,INSANI YARDIM VAFKI kutoka Uturuki, hafla iliofanyika katika Ukumbi wa Skuli ya Haile selasi mjini Unguja.
va2Baadhi ya Watoto mayatima wanaopatiwa Fedha za Msaada na I,H,H,INSANI YARDIM VAFKI kutoka Uturuki,wakishirikiana na Jumuiya ya Muzdalifat wakiongozana na walezi wao kuchukua fedha zao.Zaidi ya watoto 800,wamepatiwa fedha hizo katika ukumbi wa Skuli ya Haile Selasi mjini Unguja.
va3Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Muzdalifat Farouk akizungumza machache katika hafla ya kuwa kabidhi Fedha  Watoto Mayatima Wanao fadhiliwa na Shirika la I,H,H INSANI YARDIM VAKFI la uturuki,katika ukumbi wa  Skuli ya Haile Selasi Mjini Unguja.
va4Mfanyakazi wa Jumuiya ya Muzdalifat akiwakabidhi Watoto mayatima Wanao fadhiliwa na Shirika la I,H,H INSANI YARDIM VAKFI la uturuki,Fedha taslim za msaada katika ukumbi wa  Skuli ya Haile Selasi Mjini Unguja.
PICHA NA YUSSUF SIMAI-MAELEZO ZANZIBAR.

0 maoni:

Chapisha Maoni