Alhamisi, 16 Juni 2016

Mpango wa elimu ya biashara kwa wajasiriamali wa TBL Group waleta neema kwenye jamii.

indexWahitimu wa mafunzo ya ujasiriamali wakiwa katika picha ya pamoja katika mafunzo yaliyofanyika mkoani  Kilimanjaro hivi karibuni na kuwahusisha wenye mabaa na mameneja wao
index1Wahitimu wa mafunzo ya ujasiriamali wakiwa katika picha ya pamoja katika mafunzo yaliyofanyika mkoani  Kilimanjaro hivi karibuni na kuwahusisha wenye mabaa na mameneja wao
………………………………………………………………………………………………………………………….
-Wenye mabaa,maduka ya vinywaji na mameneja wao waupongeza
Mpango wa kuendeleza wafanyabiashara wadogo wanaouza bidhaa za kampuni ya TBL Group ujulikanao kitaalamu kama Retail Development Programme umewanufaisha ambapo idadi yao hivi sasa wanaendesha biashara zao kwa ufanisi na kuboresha maisha ya familia zao na jamii kwa ujumla.
Katika mafunzo yaliyotolewa chini ya mpango huu nchini kote baadhi ya wafanyabiashara wamepatiwa elimu kuhusiana na  usimamizi wa fedha binafsi unaolenga kumwezesha mfanyabiashara kutofautisha fedha zake na biashara ili kuepusha hasara au kufilisika, mbinu za biashara ikiwa ni pamoja na rasilimali watu na masoko.
Vipengele vingine walivyofundishwa ni uendeshaji wa biashara ya bia zinazoambatana na matangazo, kumvutia mteja kwa kuweka mazingira rafiki kwa wateja na uuzaji wa kuwajibika unaozingatia sheria za vileo, usafi na mazingira ya afya.
Wakiongea kwa nyakati tofauti kuhusiana na mpango huu baadhi ya wafanyabiashara waliohudhuria mafunzo kutoka mikoa mbalimbali nchini kwa niaba ya wenzao  walisema kuwa ni mzuri na umewawezesha kupata maarifa na mbinu za kibiashara.
Samwel Tarimo mfanyabiashara wa Mwanza akiongea kwa niaba ya wenzake waliohudhuria mafunzo hayo alisema kuwa unasaidia kuwawezesha kujua mbinu za kuleta  mafanikio katika biashara wanayofanya na kupiga hatua ya maendeleo
“Elimu inasaidia kujua mambo mengi na kuleta mabadiliko kwenye jamii na wafanyabiashara tuliohudhuria mafunzo  wengi wetu tumebadilika kuanzia kibiashara mpaka kimaisha kwa kuwa kuna mambo mengi ambayo alikuwa yanatukwamisha kibiashara hasa utunzaji wa mahesabu na kufanya mipango ya kibiashara ambayo baada ya kuyajua mafanikio ameanza kupatikana.
Naye Jane mfanyabiashara anayeuza vinywaji mkoani Arusha amesema mafunzo yalitotolewa kupitia mpango huu yamewajengea uwezo wa kujiamini katika biashara wanazofanya “Huu mpango ni mzuri na unapaswa kuigwa na makampuni mbalimbali kwa kuwa elimu tuliyopatiwa  na TBL imetufumbua macho kwa mambo mengi na wanaofuatilia masuala waliyofundishwa hivi sasa wanakwenda vizuri kibiashara.
Monica Nyaki, mfanyabiashara wa vinywaji mjini Moshi alisema licha ya kuwa na muda kwenye biashara yake lakini mafunzo hayo yamempa mbinu mpya za kujenga mahusiano mazuri na TBL, wateja na nidhamu ya pesa na usafi maeneo ya kazi na aliongeza kuwa mafanikio katika biashara yananufaisha familia nzima ya mfanyabiashara na jamii kwa ujumla.
Mkufunzi wa mafunzo hayo, Nyakahinja Manyama, alisema hivi karibuni kuwa mafunzo haya yalioendeshwa chini ya mradi wa Endelea na TBL ambao umelenga kuwawezesha wafanyabiashara wa vinywaji kujua mbinu za biashara za kuwawezesha kupata mafanikio ikiwemo kuwezesha kampuni kujenga uhusiano wa karibu na wadau wakiwemo wanaosambaza vinywaji vyake.
Pia alisema mafunzo haya ni utekelezaji wa moja ya lengo la kampuni la “kujenga dunia yenye nuru njema lenye dhamira kuongeza kasi ya ukuaji na maendeleo kwenye jamii.
“Mradi huu wa kutoa elimu ya biashara kwa wafanyabiashara wa vinywaji umeanza kuonesha mafanikio makubwa kutokana na mwitikio wa wanaohitaji mafunzo haya kuwa wengi nchi nzima na tutahakikisha tunawafikia na kuwapatia elimu hii itakayowawezesha kupata mafanikio katika biashara zao,”alisema.

0 maoni:

Chapisha Maoni