Alhamisi, 5 Mei 2016

VIJANA WAMETAKIWA KUTUMIA FURSA ZINAZOTOLEWA NA SERIKALI ILI KUONDOKANA NA HALI YA UTEGEMEZI




Afisa maendeleo ya vijana mkoa wa Iringa Atilio mganwa amewataka vijana kote nchini, kujiunga katika vikundi ili waweze kunufaika na asilimia inayotolewa na serikali kwa kila Halmshauri.

Akizungumza na mtandao wa kali ya habari   leo ofisini kwake alisema ili kupunguza wimbi kubwa la vijana wasio na ajira nchini vijana wanatakiwa kubadilika kwa kubadili mtazamo wa kususubiri kuajiliwa na hatimae kujiajiri wenyewe kwa kutumia fursa zinazotolewa na seriakali.

Atilio alisema serikali ilishatoa maelekezo kwa kila Halmashauri nchini kutenga asilimia kumi,ambapo 5% ni kwa ajili ya vijana na 5% kwa ajili ya wananwake kwa lengo la kuwainua kiuchumi.

Alisema vijana wanaonufaika na  fedha hizo ni wale waliojiunga waliojiunga katika vikundi,ambao wanapewa mikopo ya fedha na hatimae  kujiajili wenyewe kwa kufanya shughuli mbalimbali.

Alisema vijana wanapaswa kuendana na usasa kwa kujiajili wenyewe hasa katika kuchanganua shughuli za kufanya hasa katika kilimo  ambacho kinaweza kubadili maisha yao na kuachana na tabia ya utegemezi pamoja na kuaka vijiweni kupisga soga zisizo na msingi.
Ili tuweze kuendanan na kasi ya Rais Dkt Magufuli vijana tunatakiwa tufanye kazi kwa bidii zaidi  kila mmoja kwa nafasi yake mahali alipo  ili kuunga mkono juhudi zinazofanywa na serikali ya awamu ya tano.

Atilio alisema pamoja na hayo vijana wanakabiliwa na changamoto  kubwa ya uhaba wa maeneo ya kuendeshea shughuli zao kama kilimo na biashara kutokana na Halmashauri pamopja na serikali za vijiji kushindwa kutenga eneo maalumu kwa ajili ya vijana na hatimae kukodi na kushindwa kumudu gharama hizo

Vijana wanashindwa kuendesha shughuli zao kwasababu ya kutotengewa nmaeneo yao maalumu,Hali hii inasababisha kushindwa kufanya kazi zao hasa katika kilimo na biashara.Asilimia kubwa ya vijana nchini wako vijjijini na wanategemea kilimo na biashara ndogondogo,hivyo serikali kwa kupitia Halmashauri zetu inatakiwa kuona umuhimu wa kutenga maeneo maalumu kwa ajili ya vijana ili waweze kuendesha shughuli zao ya vijanan walio’’’’’’’ alisema
Kutokana na hali hiyo tumepanga mikakati kwa mkoa mzima kwa pamoja tumeshawishi kila Halmashauri ifungue SACOS  ya vijana ili na tayari zimefunguliwa katika wilya ya Mufindi,Kilolo,Iring mjini,Iringa vijijini na katika Halmashauri ya Mji wa Mafinga Mchakato wa ufunguzi unaendelea’’’’’alisema
Alisema sacos hizo zitasaidia  waliopo katika vikundi kjipatia fedha na kujiajili wenyewe,hali itakayosaidia kujiajili na kuachanan na utegemezi na kusubiri kuajiliwa na serikali pekee.
Kama unavyojua vijana waliowengi wanafikiri serikali pekee ndiyo inayoweza waletea maendeleo yao binafsi baada ya kuajiliwa wakati kuna fursa nyingi hasa katika kilimo,kwani vijana wengi wanadhani swala la kilimo ni la wazee tu.wakati ni sasa ambapo watanzania tunatakiwa kuamka’’’’’alisema
Aidha aliwaasa vijana kujiepusha na maradhi ya kuambukizwa ambayo yanaweza waletea madhara ya kiafya na kushindwa kuendeleza shughuli zao za kimaendeleo kwa manufaa yao na Taifa kwa ujumla.



0 maoni:

Chapisha Maoni