Kwa Habari za kitaifa na kimataifa

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za michezo na burudani

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za afya

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za Kilimo

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za uchumi na biashara

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za elimu

Tembelea Kali ya habari

Jumamosi, 30 Julai 2016

AfDB yaahidi kuendelea kuipiga jeki Tanzania kukuza uchumi wake


Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango, amekutana na kufanya  mazungumzo na Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Frannie Leautier, ofisini kwake jijini Dar es Salaam, ambapo ameishukuru Benki hiyo kuwa mojawapo ya mashirika ya kimataifa yanayoisaidia Tanzania katika sekta mbalimbali za maendeleo.
Benki hiyo imewekeza hapa nchini kiasi cha dola Bilioni 2 sawa na zaidi ya shilingi Trilioni  4.4 kama ruzuku na mikopo yenye riba nafuu ili kuendeleza sekta mbalimbali ikiwemo barabara, elimu, kilimo, nishati ya umeme, na viwanda.
Katika mazungumzo hayo Mhe. Dkt. Mpango, ameelezea kufurahishwa kwake na Dira ya AfDB ambayo inafanana na vipaumbele vya serikali, kupitia Mpango wa Pili wa Taifa wa Maendeleo wa miaka mitano ambao umelenga kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda ifikapo mwaka 2025.
Dira ya Benki hiyo imejikita katika malengo matano ambayo ni kuwekeza katika nishati ya umeme, uzalishaji wa chakula, kuendeleza viwanda, kuiunganisha Afrika kwa mtandao wa barabara na kuboresha maisha ya watu.  
Dkt. Philip Mpango
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango (kulia) akiwa kwenye majadiliano na Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Frannie Leutier (katikati) na Mwakilishi mkazi wa Benki hiyo Bi. Tonia  Kandiero.
Mhe. Dkt. Mpango, amesema kuwa uwekezaji katika sekta hizo utasaidia mpango mkubwa wa uboreshaji wa miundombinu kama vile kujenga viwanda kwa kuhusisha sekta ya umma na binafsi-PPP, umeme wa kutosha kuendesha viwanda, barabara ambazo zitaunganisha nchi zote  za Afrika.
“AfDB wametusaidia sana katika ujenzi wa barabara nyingi nchini Tanzania ikiwemo barabara ya kutoka Tanga kwenda Horohoro, ambayo imerahisisha usafiri wa kwenda nchini Kenya.  Barabara nyingine zitajengwa kutoka mpakani Kagera kupitia Kigoma kwenda Katavi, Dodoma hadi Iringa.  Hili ni jambo kubwa” Alisema Dkt. Mpango
Dkt. Mpango amemweleza Makamu huyo wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika-AfDB, Dkt.  Frannie Leautier juu ya mpango wa serikali wa kuimarisha sekta ya usafirishaji ikiwemo kujenga Reli ya Kati kwa kiwango cha Kimataifa (standard gauge) ambapo kiasi cha shilingi Trilioni 16 kinahitajika kukamilisha mradi huo.
Ameeleza kuwa tayari serikali imetenga kiasi cha shilingi Trilioni 1 katika bajeti yake ya mwaka huu 2016/2017 kwaajili ya kuanza kutekeleza mradi huo mkubwa unaohusisha njia ya reli yenye urefu wa kilometa 2,190.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango akifafanua jambo mbele ya Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB ) Dkt. Frannie Leutier, kulia kwa Dkt. Leutier, ni Mwakilishi mkazi wa Benki hiyo Bi. Tonia  Kandiero na watendaji wa Wizara.
Ameitaja Sekta nyingine ya kipaumbele kuwa ni kilimo kwaajili ya kuzalisha chakula kwa wingi kwaajii ya kutosheleza matumizi ya ndani na ziada yake kuuzwa nje ya nchi huku ikitiliwa mkazo uzalishai wa malighafi zitakazotumika katika viwanda.
Katika mazungumzo hayo Waziri wa Fedha na Mipango alimpongeza Dkt. Leautier, ambaye ni raia wa Tanzania, kwa kupata nafasi ya Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika AfDB, kuwa ni faraja na kielelezo kizuri kwa akina mama wa Kitanzania kuwa wanaweza.
Kwa upande wa Makamu wa Rais wa AfDB Dkt. Frannie  Leautier Dkt. Leautier, ambaye aliambatana na Mwakilishi mkazi wa Benki hiyo hapa nchini, Bi. Tonia Kandiero, amesema kuwa AfDB imesaidia na itaendelea kusaidia  miradi mingi ya maendeleo hapa nchini ikiwemo ya barabara, elimu, kilimo, afya, sekta ya umeme ili Tanzania iwe na umeme wa kutosha kuendesha viwanda.
“Kwa kufanya hayo uchumi wa nchi utaimarika, vijana watapata ajira, wananchi watakuwa na maisha bora, chakula kitazalishwa cha kutosha na kingine kuuzwa nje ya bara la Afrika, Viwanda vitasaidia sana kiumarisha uchumi wa nchi kwani bila viwanda ni vigumu sana kuendelea” alisema Dkt. Leautier

Dkt Mpango
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango, akitoa ufafanuzi kuhusu vipaumbele vya Serikali ya awamu ya tano kwa Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB ) Dkt. Frannie Leutier (Hayupo pichani).
Ameahidi kuwa Benki yake itaendelea kusaidia kuinua sekta ya kilimo kupitia Benki ya Maendeleo ya Kilimo kwa kutoa mkopo wenye masharti nafuu ili kuwawezesha wakulima wakubwa, wa kati na wadogo kupata fursa ya mikopo hiyo itakayosaidia uzalishaji wa mazao.
Dkt. Leautier amesema kuwa atawasilisha kwenye bodi ya benki hiyo wazo la Tanzania kutaka kupigwa jeki katika ujenzi wa Reli ya Kati kwa kiwango cha kimataifa kwa kuwa mradi huo utakuwa na manufaa makubwa si tu kwa Tanzania, bali kwa nchi zote zinazoizunguka zikiwemo zile ambazo hazina bahari.
“Mradi huo ukikamilika utasaidia pia kunusuru barabara ambazo zimekuwa zikiharibika kutokana na kupitishwa mizigo mingi mizito ambayo ingefaa kusafirishwa kwa njia ya reli ili kuzifanya barabara hizo zidumu muda mrefu” aliongeza
Benki ya Maendeleo ya Afrika AfDB, kupitia mfuko wake wa Maendeleo-African Development Fund (ADF),  imeahidi kutoa kiasi cha Dola Milioni 200, sawa na shilingi 433.6 bln,  kama ruzuku na mkopo wenye masharti nafuu kwenye Mfuko Mkuu wa Bajeti wa serikali katika kipindi cha mwaka wa fedha 2017/2018.
Imetolewa Benny Mwaipaja, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano – Wizara ya Fedha na Mipango
Mwakilishi mkazi wa Benki hiyo Bi. Tonia Kandiero
Mwakilishi mkazi wa Benki hiyo Bi. Tonia  Kandiero (wa kwanza kushoto) akitoa ufafanuzi kwa Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango. Kutoka kushoto kwake ni Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB ) Dkt. Frannie Leutier, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Benny Mwaipaja (anayeandika).
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango akiagana na Mwakilishi mkazi wa Benki hiyo Bi. Tonia Kandiero.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango akiagana na Mwakilishi mkazi wa Benki hiyo Bi. Tonia  Kandiero.
Dkt. Frannie Leutier
Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB ) Dkt. Frannie Leutier akisoma jambo kwenye kompyuta ndogo wakati akieleza jambo kwa Mhe. Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, alipomtembelea na kufanya mazungumzo naye ofisini kwake Jijini Dar es salaam.
Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB ) Dkt. Frannie Leutier
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango akiagana na Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB ) Dkt. Frannie Leutier.

Serikali imetoa ujumbe huu kwa wasanii, wasiofata ya Nay Wa Mitego kuwakuta


pix 12
Wasanii nchini wameaswa kuzingatia maaadili katika utengenezaji wa kazi zao ili kuenzi na kulinda mila, desturi na tamaduni za mtanzania .
Wito huo umetolewa jana na Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura wakati akizindua studio ya kisasa ya kurekodi kazi za sanaa ya Wenene Entertainment.
Mhe Anastazia Wambura amesema kuwa baadhi ya wasanii wamekuwa hawafati maadili katika utengenezaji wa kazi zao na kuvifanya vyombo vinavyosimamia kazi za sanaa nchini kama Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) kutoa adhabu dhidi yao kutokana na ukiukwaji wa maadili katika kazi zao.
“Ninaiomba kampuni ya Wanene Entertainment kuisaidia Serikali kuwaelimisha wasanii watakaoleta kazi zao kutengenezwa kwenu kuzingatia maadili badala ya kutengeneza kazi ambazo haziendani na maadili ya nchi yetu” alisema Mhe Anastazia.
Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Bibi. Joyce Fissoo amehaidi kushirikiana na studio ya Wanene Entertainment kuendeleza sanaa ya Tanzania kufikia katika viwango vya kimataifa na kuongeza pato la wasanii na taifa kwa ujumla.
Naye Mkurugenzi wa kampuni ya Wanene Entertainment Bw. Darsh Pandit amesema kuwa ufunguzi wa studio hiyo ni muitikio wao kwa Serikali ya awamu ya tano katika suala la kutoa ajira kwa vijana na kuwezesha vijana kujiajiri kwa kutumia vipaji vyao kupitia kazi za sanaa.
“Studio hii ina lengo la kukuza na kuendeleza sanaa ambayo imekuwa ajira kubwa kwa vijana wengi na tunaahidi kuzingatia maadili katika utengenezaji wa kazi zetu na pia tutazingatia ubora ili kuitangaza sanaa ya Tanzania kimataifa” alisema Bw. Pandit.

Alhamisi, 28 Julai 2016

Dk. Kigwangalla akutana na Wakuu wa Idara za Maendeleo ya Jamii, Watoto atoa maagizo


Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangalla amekutana na Wakuu wa Idara za Maenedeleo ya Jamii pamoja na ile ya Watoto katika Wizara hiyo na kupanga mikakati mbalimbali ya kiutendaji kazi.
Katika tukio hilo, Dk. Kigwangalla amewataka wakuu hao wa Idara kuhakikisha wanaandaa mpango kazi kabambe ili kuongeza ufanisi wa utendaji kazi ndani ya Wizara hiyo ikiwemo kutoa maagizo maafisa Maendeleo ya na Ustawi wa Jamii kuhakikisha wanatoka maofisini na kwenda ngazi ya chini kufanya kazi hasa Vijijini.
Pia katika kukabiliana na suala la mmong’onyoko wa maadili hasa suala la vitendo vya watu kujihusisha na mapenzi ya Jinsia moja, amebainisha kuwa mikakati hiyo kwa sasa wataanzia ngazi ya chini katikakuhakikisha wanadhibiti vitendo hivyo.
“Tunataka kuhakikisha vitendo vya unyanyasi na ukatili hasa vile vinavyoanzia mashuleni tunavikomesha mara moja. Imebainika zipo baadhi ya shule watoto wanafanya vitendo visivyo fa ambavyo pia baadae vinapelekea tabia hii ya ushoga.
Hivyo miongoni mwa mikakati ni kuhakikisha tunaandaa masunduku ya maoni kwa kila shule ili kubaini vitendo hivi na vingine visivyofaa kwa Wanafunzi ambavyo vinapelekea mmong’onyoko wa maadili.” Alieleza Dk. Kigwangalla.
Dk. Kigwangalla amekutana na wakuu hao ni katika mikakati ya kuhakikisha anasimamia ipasavyo  majukumu ya Idara hizo ambazo zinaunda Wizara hiyo.
DSC_3248Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangalla akipitia madokezo mbalimbali ya Idara za  Wizara hiyo muda mfupi kabla ya kukutana na Wakuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii na ile Idara ya Watoto.
DSC_3261Afisa wa Idara ya Watoto, Emmanuel Batoni akielezea jambo kwa Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangalla (Hayupo pichani) wakati wa tukio hilo lililofanyika katika ukumbi wa Wizara hiyo.
DSC_3275Mkutaano huo wa Naibu Waziri na Wakuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii na ile ya Watoto ukiongozwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangalla DSC_3279 DSC_3288
Sehemu ya Wakuu wa Idara za Maendeleo ya Jamii wakimsikiliza Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangalla
DSC_3295 DSC_3289
DSC_3281Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangalla akitoaa maagizo kwa Wakuu wa Idara mbalimbali wa Wizara hiyo.(Picha zote na Andrew Chale,).

MWALIMU WA SHULE YA MSINGI WILAYANI LUDEWA MATATANI KWA KUBAKA WANAFUNZI WAKE .......

Esta Malibiche on July 28


MWALIMU Abute Fungo (40 ) wa shule ya msingi Kimelembe kata ya Nkomang’ombe Ludewa mkoani Njombe pichani  atiwa mikononi mwa polisi Ludewa kwa tuhuma za kubaka na  kuwapiga picha sehemu za siri wanafunzi wake  zaidi wanne  na  kuwalipa kati ya Tsh 500  na  1000
“Mwalimu amenilazimisha kufanya nae mapenzi  zaidi ya mara nane na alikuwa akinilazimisha kumeza dawa za majira akiniambia kuwa zinazuia mimba hata hivyo nilikuwa nameza bila kutumia maji”.alisema mtoto mmoja wa  watoto  hao

Watoto  hao  walisema  kuwa mwalimu  wao  huyo alikuwa akiwafanyia  vitendo  hivyo kwa nyakati tofauti  katika vichaka vilivyopo jirani na  kanisa la kiinjili la Kilutheri Tanzania katika kijiji cha Kimelembe Kata ya Mkomang’ombe.
Wakizungumza mtandao huu  wa  matukiodaimaBlog  watoto wanne walioamua kutoa ushuhuda wao kabla na baada ya kufika polisi walisema mwalimu amekuwa akitenda unyama kwa  wanafunzi kila mwaka na kuongeza kuwa wenzao zaidi ya nane walishabakwa kwa kipindi cha mwaka jana na wazazi wachache kulipana nje ya mahakama.

Watoto hao wenye umri chini ya miaka 14 waliongeza kuwa mwalimu alikuwa akiwalipa pesa kati ya sh500 hadi 1000 kama malipo kabla na baada ya kufanya kitendo hicho polini.
Kamanda wa polisi Mkoa wa Njombe Kamishna Pudenciana Protas amekiri kukamatwa kwa mwalimu huyo na kwamba mtuhumiwa atafikishwa mahakamani wakati wowote kuanzia sasa. 
Watoto hao ambao ni wanafunzi wa darasa la saba katika shule ya msingi Kimelembe wilayani hapa walisema kuwa ubakazi huo umefanya kwa muda mrefu na mwalimu huyo lakini wamekuwa wakishindwa kutoa taarifa kwa wazazi wao na walimu wengine kutokana na kuogopa vitisho kutoka kwa mwalimu huyo.
Walisema kuwa mwalimu huyo amekuwa akitoa adhabu kali kwa mwanafunzi anayekataa kufanya naye tendo hilo hiyo imekuwa inawapa wakati mgumu wanafunzi kukataa kufanya hivyo wakihofia kuzalilishwa kwa adhabu kali mbele ya wanafunzi wengine.
Wanafunzi hao walisema kuwa walianza kuitoa siri hiyo kwa mama yao mdogo wakati wakifua nguo za shule katika mto nchuchuma ndipo mama yao mdogo huyo alipoamua kuwaeleza wazazi wao na kuchukua uamuzi wa kulipeleka jambo hilo katika Serikali ya Kijiji.
Walisema baada ya uongozi wa kijiji kupata taarifa hiyo ndipo wakaamua kutoa taarifa katika jeshi la Polisi ambapo jeshi la polisi liliamuru kukamatwa kwa mwalimu huyo na kufikishwa Mahakamani.

Jumatano, 27 Julai 2016

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI MWIGULU NCHEMBA ATUA KATIKA MGODI WA NYAMHUNA UNAODAIWA KUUA MTANZANIA

Postedy by Esta Malibiche on July 27.2016 in News with No comment
 









Picha na Festo Sanga


Waziri wa mambo ya ndani ya Nchi,Mwigulu Nchemba leo hii amewasili katika mkoa wa Geita  kwa ziara ya kikazi .
Waziri katika ziara yake amembelea  Mgodi wa Nyamhuna unaodaiwa kuwa, raia wa china ambao ni sehemu ya wamiliki wa mgodi huo wakishirikiana na watanzania walimtesa kinyama na kumjeruhi mmoja wa mtanzania mwenzetu aliyekuwa akifanya kazi katika mgodi huo uliopo Katoro-Geita.
 '''''''Imenilazimu kufika gereza la Geita kukutana na kijana huyo ambae yupo hai tofauti na taarifa za awali kuwa alifariki.Baada ya kujiridhisha kuanzia mavazi,majeraha,picha,sura na umbo lake kuwa ndiye kijana aliyeteswa vibaya na picha zake kusambaa mitandaoni na vyombo mbalimbali vya habari''''alisema Mwigulu
''''''Niliamua kwenda naye hadi mgodini lilipofanyika tukio hilo la kinyama,aliwatambua wahusika ambao walishiriki kufanya tukio hilo la kinyama  ambalo halikubarika hapa nchi''''''....alisema Mwigulu
Alisema  walioshiriki tukio hilo wanashikiliwa na jeshi la polisi, tayari kwa kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.
Aidha Waziri Mwigulu alisema amesikitishwa na kitendo hicho,kilichofanywa na waamiliki wa mgodi huo na kulaani vikali.Pia alisema ,serikali  ipo tayari kushirikiana  rai wema watakaofichua na kutoa taarifa popote pale zinazohusu  matukio au viashiria  vinavyohatarisha usalama  wa wananchi

"Usalama wetu,jukumu letu sote"





RAIS DKT. MAGUFULI AWAAPISHA MWENYEKITI PAMOJA NA KATIBU WA TUME YA UTUMISHI WA WALIMU (TSC) IKULU CHAMWINO MKOANI DODOMA

chm1Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Oliva Joseph Mhaiki kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) Ikulu ndogo ya Chamwino Mkoani Dodoma.
chm3Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Winfrida Gaspa Rutaindurwa kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) Ikulu ndogo ya Chamwino Mkoani Dodoma.
chm5Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) Oliva Joseph Mhaiki (kushoto) pamoja na Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) Winfrida Gaspa Rutaindurwa (kulia) mara baada ya kuwaapisha ) katika  Ikulu ndogo ya Chamwino Mkoani Dodoma.
chm6Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) Oliva Joseph Mhaiki (watatu kutoka kushoto) pamoja na Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) Winfrida Gaspa Rutaindurwa (watatu kutoka kulia) mara baada ya kuwaapisha. Wengine katika picha ni Waziri Mkuu Kassim Majaliwa , Mwanasheria Mkuu wa Serikali George Masaju, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi na Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI Seleman Jafo.
chm7Rais Dkt. John Magufuli akisalimiana na Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI Seleman Jafo mara baada ya tukio la uapisho katika  Ikulu ndogo ya Chamwino Mkoani Dodoma. Katikati ni Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.
chm8Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akimpongeza Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) Oliva Joseph Mhaiki mara baada ya tukio la uapisho wa Mwenyekiti huyo pamoja na Katibu wa Tume hiyo katika Ikulu ndogo ya Chamwino Mkoani Dodoma. Picha na IKULU

PSPF YAMKABIDHI KIASI CHA TSH.8 MILL. MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA KONDOAKWA AJILI YA MADAWATI




Picha kutoka maktaba ya Mkurugenzi

 Mkurugenzi wa  Halmashauri ya wilaya ya kondoa Mkoani Dodoma  Falessy Kibasa amepokea leo hii mchango wa Madawati  kiasi cha Mill.8 kutoka  shirika la Taifa la hifadhi ya jamii PSPF  ,pamoja na mashuka 200 kwa ajili ya hospitali





Kampuni ya TBL kuendelea kufanikisha utoaji elimu ya usalama katika jamii

JIS1Afisa Mwandamizi kutoka Kitengo cha Elimu katika Jeshi la Polisi kikosi cha usalama barabarani , ASP. Mossi Ndozero akitoa Elimu ya usalama barabarani kwa baadhi ya walimu wa shule za Mkoa wa Mwanza yaliyofanyika katika Chuo cha Polisi Wanamaji jijini Mwanza yaliyoendeshwa na jeshi hilo chini ya udhamini wa kampuni ya TBL Group.
JIS2SGT Bahati Nzunda akitoa somo kwa walimu wakati wa mafunzo hayo.
JIS3 JIS4Baadhi ya walimu wakifanya mazoezi katika makundi
JIS5Walimu wakifuatilia mafunzo ya usalama barabarani
…………………………………………………………………………………………………….
Kampuni ya TBL Group imetangaza  kuwa itaendelea kutoa elimu ya Usalama katika maeneo yake ya kazi na kwa jamii ili kuhakikisha matukio ya ajali zisizo za lazima zinapungua hapa nchini.
Hayo yamebainishwa na  Meneja wa Usalama kazini wa kiwanda cha  TBL cha mjini Mwanza,Bw.Method Marco  wakati akielezea mafunzo ya usalama ambayo yamefadhiliwa na kampuni kwa ajili ya walimu wa shule za msingi na sekondari na wakaguzi wa magari kutoka Jeshi la polisi nchini mkoani humo.
Bw.Method alisema linapokuja suala la usalama na afya haliwahusu wafanyakazi wa kampuni na familia zao tu bali kwa jamii nzima kwa kuwa wafanyakazi wa TBL Group ni sehemu ya jamii  na wanaishi kwenye jamii.
“Sera za kampuni yetu zinahimiza kulipa kipaumbele mkubwa suala la Usalama na afya sio kwa wafanyakazi tu bali usalama wa jamii nzima na ndio maana kampuni imekuwa mstari wa mbele kufadhili na kushiriki katika kampeni mbalimbali za usalama na miradi ya Afya na Mazingira”.Alisema Marco.
Kuhusiana na ufadhili wa  semina ya wakaguzi wa magari kutoka Jeshi la polisi  na walimu wa shule  za msingi na ekondari alisema kuwa kampuni imekuwa ikifanya kazi kwa karibu na taasisi hizo kuhusiana na masuala ya usalama hususani kampeni za usalama barabarani lengo kubwa likiwa ni kupunguza matukio ya ajali nchini.
Moja ya lengo lengo letu tunalotekeleza ni kuhamasisha unywaji wa kistaarabu kwa jamii hivyo kama kampuni inayotengeneza vinywaji tunalo jukumu la kuelimisha masuala ya usalama kwa ujumla na tunaamini Jeshi la polisi kama msimamizi wa masuala ya usalama barabarani nchini linapaswa kuungwa mkono na kupewa ushirikiano mkubwa kuhakikisha linafanikisha kufikisha elimu ya usalama na usalama barabarani kwa wananchi wengi.
Kwa upande wa walimu na wanafunzi alisema kuwa kampuni itaendelea kushirikiana nao  ikiwemo wadau wengine kuhakikisha  wanapata elimu ya usalama barabarani “Ukifundisha walimu ni rahisi elimu hii kuwafikia wengi na wanafunzi wakipata elimu ya awali ya masuala ya usalama na usalama barabarani wanakua wakiwa na uelewa mpana wa kujikinga na kuchukua tahadhari.
Alisema suala la kuelimisha jamii kuhusiana na usalama barabarani ni  jambo ambalo kampuni ya TBL Group itaendelea kulivalia njuga kwa nguvu zote kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi na wadau wengine