Jumatatu, 13 Juni 2016

WATUMISHI HEWA169 IRINGA WATUMIA MILL.364




Serikali mkoani hapa imetangaza orodha mpya ya wafanyakazi hewa 169 katika Halmashauri zote tano za mkoa huo ambao wameisababishia serikali hasara  ya Sh .364.02
Ongezeko la idadi hiyoinafanya Mkoa wa Iringa kuwa na jumla ya watumishi hewa 197 baada ya taarifa za awali kueleza uwepowa watumishi 27 hewa mkoani hapa.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini hapa jana mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Masenza alisema watumishi hao wamegawanyika katika makundi matatu ambayo ni kundi la wasitaafu,watoro na waliofarikiambao waliendelea kulipwa mishahara.
“Mtakumbuka kuwa April 18 mwaka huu  nilitoa taarifa ya idadi ya wafanyakazi hewa 21 lakini nikaeleza kuwa ninaunda timu ya wataalam kuchunguza jambo hili ili  kujiridhisha na kuondokana kabisa na tatizo la watumishi hewa mkoani hapa”alisema Masenza na kuongeza:
“Timu  niliyounda imemaliza kazi na kunikabidhi ripoti Juni 7 mwaka huu  ,kwa ufupi ni kwamba timu imegundua uwepo wa wafanyakazi hewa 169 katika halmashauri zote tano za mkoani hapa,pia watumishi hao  wameisababishia serikali hasara ya Sh 364,028,910.80”alisema.
Sambamba na watumishi hewa Mkuu huyo wa mkoa alibainisha tatizo lingine lililoibuliwa na timu yake ya wataalamu kuwa  ni suala la matumizi mabaya ya fedha zaserikali yaliyofanywa na uongozi wa hosptaliya Teuli ya  Ilula  inayotoa huduma katika Wilaya ya Kilolo.
 
Alisema  timu hiyo libaini matumizimabaya ya Sh 151,583,969.00 ambalo alidai lilikuwa la mishara isyolipwa na hazikurejeshwa hazina tangu mwaka 2008 hadi februari 2016..
“Fedha hizo ambazo kisheria ilibidi zirejeshwa hazina zilitumika kugharamia shughuli za uendeshaji wa hosptali hiyo ikiwamo kulipa mishara watumishi ambao orodha yao haijajuloikana serikalini,kununu dawa na kulipiagharama za umeme  pasipo idhini ya serikali”alisema Masenza.
Masenza alisema serikali inaendeela na uchunguzi dhidi ya jambo hio na hatua zitachukuliwa ikwia ni pamoja  na kufanyia kazimapendekezoya ripoti ya wataalamu.
Akizunguzia suala la watumishi hewa serikali  imejipanga kuchukua hatua dhidi ya watumishi wote waliohusika na kusababishia uwepo wa watumishi hewa waliosababuishia serikali hasara ya kiasi hicho cha fedha.
Akizungumzia suala hilo mkazi wa Iringa Ramadhan Mahano alipongeza serikali ya mkoa kuweza kubainisha watumishi hewa na kuishauri kulifanya jambohilo kuwa la kudumu ili kulifanya tatizo  lawatumishihewakutojirudia.
“Wanaochangia uwepo wa watumishi hewa ni watumishi pia niombe serikali ifafanya uchunguzi wa kina na wahusika wote wafikishwa mahakamani ili haki iweze kutendeka, kwakufanya hivyo kutasaidia kuondoa tatizo hilo kabisa”alisema Mahano.
Katika hatua nyingine  mkuu huyo wa mkoa alisema bidhaa ya sukarimkoani hapaimeadimika na kwamba kampuni ya Mohamed Intrepraise LT D inatarajia kuingiza sukarihiyokuanzia leo.
“Sukaria imeadimika na imepanda bei kutoka Sh 1800 ya zamani hadikufikia 2800 na3000,Iringa  hatuna kiwanda cha sukari na sukariinayotumika hapani kutoka nje ya mkoa wa Iringa,kwa sasa msihofu serikaliyenuimechukuahatua ya kuyaomba makampuni makubwa kuleta sukari kuanzie (kesho) leo”alisema         Masenza.
 

0 maoni:

Chapisha Maoni