Ijumaa, 10 Juni 2016

Miundombinu ya umeme kuboreshwa Bagamoyo


tae1Kaimu Kamishna wa Nishati anayeshughulikia umeme,Mhandisi Leornard Masanja( wa pili kulia) akikagua baadhi ya trasfoma zilizobiwa mafuta katika ofisi ya Tanesco wilayani Bagamoyo, kulia ni Meneja wa Tanesco Mkoa wa Pwani, Mhandisi Martin Madulu na Meneja Tanesco Wilaya ya Bagamoyo ( kushoto )
tae2Baadhi ya transfoma zilizoibwa mafuta zikiwa katika ofisi ya Tanesco  Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani.
tae3Kaimu Kamishna wa Nishati anayeshughulikia umeme,Mhandisi Leornard Masanja( wa pili kulia) akikagua baadhi ya trasfoma zilizobiwa mafuta katika ofisi ya Tanesco wilayani Bagamoyo, kulia ni Meneja wa Tanesco Mkoa wa Pwani, Mhandisi Martin Madulu na Meneja Tanesco Wilaya ya Bagamoyo ( kushoto )
………………………………………………………………………………………………………………..
Na Zuena Msuya, Bagamoyo Pwani
Wizara ya Nishati na Madini imesema itaendelea kuimarisha miundombuni ya upatikanaji wa huduma ya umeme wilayani Bagamoyo mkoani Pwani ili kuondoa malalamiko ya mara kwa mara yanayotolewa na wateja.
Kaimu Kamishna wa Nishati anayeshughulikia umeme, Mhandisi Leornard Masanja alisema hayo wilayani Bagamoyo baada ya kufanya ziara katika Ofisi ya shirika la umeme nchini (Tanesco) hivi karibuni.
Akiwa katika ziara hiyo, Mhandisi  Masanja alielezwa kuwa transfoma 56 ziliibwa mafuta na kusababisha wananchi wengi kulalamikia Tanesco kwa kuchelewa kuwapatia huduma ya umeme licha ya kukamilisha hatua zote za kuunganishwa na huduma hiyo na umeme kukatika mara kwa mara.
Pia alielezwa kuwa, Tanesco imekuwa ikichelewa kutatua changamoto zinazowakabili wananchi wa maeneo hayo pindi inapotokea hitilafu ya umeme au kukatika kwa huduma ya umeme katika eneo fulani la Wilaya na Mkoa huo.
Baada ya kupokea malalamiko hayo, Mhandisi Masanja aliwataka Meneja Tanesco, Mkoa wa Pwani Mhandisi Martin Madulu pamoja na Meneja wa Wilaya ya Tanesco wa Wilaya ya Bagamoyo, Mhandisi Julius Doyi kutoa ufafanizi wa namna ya kukabiliana na changamoto hizo pamoja na kutatua malalamiko hayo kutoka kwa Meneja Tanesco, Mkoa wa Pwani Mhandisi Martin Madulu pamoja na Meneja wa Wilaya ya Tanesco Wilaya ya Bagamoyo, Mhandisi Julius Doyi.
Kwa upande wake Meneja Tanesco, Mkoa wa Pwani Mhandisi Martin Madulu, alisema kuwa malalamiko hayo yanatokana na uchache wa miundombinu hasa kwa wale wanaohitaji kuunganishiwa huduma ya umeme.
Aidha alifafanua kuwa watumishi wachache waliofukuzwa wamekuwa wakidaiwa kuhujumu shughuli nzima za kuunganisha huduma za umeme kwa wananchi kwa kudai rushwa kwanza jambo lililokuwa likiwakatisha tamaa wananchi.
Hata hivyo alielezwa kuwa, tayari wafanyakazi wanane wamefukuzwa kazi wilayani bagamoyo kwa makosa mbalimbali ikiwemo rushwa,matumizi mabaya ya ofisi na kuchelewesha huduma kwa wananchi.
Naye Meneja wa Tanesco wilayani Pwani Mhandisi Julias Doyi alisema kuwa tatizo la kuchelewa kuwahudumia wananchi hasa wale wanaopata tatizo la kukatika huduma ya umeme linatokana na miundombinu mibovu ya kuwafikia wananchi hao na kuwa na Gari moja la kutoa huduma kwa wilaya nzima.
Aliongeza kuwa Tanesco wamekuwa wakichelewa kupata taarifa kutoka kwa wananchi kutokana na wengi wao kutoa taarifa hizo kupitia Viongozi wa Serikali za mitaa na kusababisha taarifa hizo kuchelewa kuwafikia Tanesco.

0 maoni:

Chapisha Maoni