Ijumaa, 4 Novemba 2016

PILI SHING'OMA;AKEMEA KUWANYANYAPAA WALEMAVU WA NGOZI, ALBINO



 Posted by Esta Malibiche on Nov 4,2016 in NEWS
 
 Dkt.wa Magonjwa ya Ngozi na via vya uzazi Pili Shing'oma akitoa Elimu kuhusu matumizi ya mafuta .Pia alitoa Elimu kwa wazazi wenye mtazamo tofauti kuhusu watoto wanaozaliwa na ulemavu wa ngozi na kusema kuwa ,wazazi wanaweza kuwa weusi lakini wakawa na vina 7 vya ualbino,hii haikwepeki.Alisema anawashangaa baadhi ya wazazi kuwatenga watoto wanaozaliwa na ulemavu wa ngozi na kuwanyanyasa wanawake wanaojifungua watoto wenye ulemavu wa ngozi.


 Pendo Kilezu Muuguzi na mtoa huduma kwa walemavu wa ngozi katika Hospital ya Rufaa mkoa wa Iringa,akitoa Elimu jinsi ya matumizi ya mafuta ya ngozi kwa walemavu wa ngozi Albino,aliwataka na kusema kuwa, kumekuwa na wimbi kubwa la baadhi ya wazazi kuwaficha watoto ndani wenye ulemavu wa ngozi Albino,na hatimae kushindwa kuwapatia matibabu na mahitaji muhimu yanayostahili kama binadamu wengine.

 Pendo Kilezu Muuguzi na mtoa huduma kwa walemavu wa ngozi katika Hospital ya Rufaa mkoa wa Iringa,akiendelea na zoezi la kutoa Elimu juu ya kupaka mafuta.


Katibu wa chama cha watu wenye ulemavu wa Ngozi [TAS]Mkoa wa Iringa Leonansi Sambala alilishukuru shirika la USAID kwa kuwapatia vifaa vinavyosaidia watu wenye ulemavu wa ngozi kujikinga na mionzi ya jua ambayo inaweza letya athari kubwa kwao wakati wakifanya shughuli za maendeleo pamoja na wanafunzi.
Salome Kanyika ni mmoja wa wazazi mwenye watoto wenye ulemavu wa ngozi Albino,aliisihi jamii kutowatenga watoto wenye ulemavu wa ngozi kutokana na dhana ya baadhi ya makabila na kooo kusema kuwa motto akizaliwa na ulemavu wa ngozi inakuwa ni balaa katika familia,na kusisitiza kuwa mtoto mwenye ulemavu wa ngozi ni sawa na binadamu wengine na anastahili kupata haki zake za msingi.

Mashaka Mjilima ni baba wa Peter Mashaka ambae yeye na mke wake wote ni weusi lakini wanavina 7 vya ualbino,aliitaka jamii kuachana na tabia ya kuwakata viungo watu wenye ulemavu wa Ngozi kwa imani za kishikrikina wakidhani watapata utajirii.Huo ni uongo unaofanywa na waganga wa jadi ili kujiiingizia kipato kwa ajili ya kujikimu kimaisha na kusababisha  walemavu kutoishi kwa Amani katika Nchi yao.



 




 


 


Picha zote na Esta Malibiche [KALI YA HABARI BLOG]

Na Esta Malibiche

Iringa

Wazazi wametakiwa kutowaficha watoto wenye ulemavu wa ngozi Albino,bali wawapeleke katika vituo vya Afya ili waweze kupata matibabu pamoja na vifaa vyakujikinga na jua ili wasiweze kuathirika na mionzi ya jua.


Hayo yamesemwa jana na Daktari wa magonjwa ya Ngozi na via vya Uzazi  Dkt.Pili Shing’oma wakati wa  akitoa Elimu  kwa wazazi na watu wenye ulemavu wa ngozi juu ya kujikinga na Saratani ya Uzazi na Clinic ya watu wenye ulemavu wa Ngozi uliofanyika  jana katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Iringa.

Sheng’oma alisema kuwa kumekuwa na wimbi kubwa la baadhi ya wazazi kuwafika watoto ndani yenye ulemavu wa ngozi Albino,na kushindwa kuwapatia matibabu na mahitaji muhimu yanayostahili kama binadamu wengine.


Alisema kumekuwa na vitendo vya kikatili na unyanyasaji usiostahili dhidi yao walemavu wa ngozi kuuawa na wengine kutengwa na familia zao kutokana na ulemavu huku baadhi ya wananchi wakishiriki mambo ya kishirikina kuwakata baadhi ya viongo.

Alisema wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa usafiri na nauli ili kuwafikia walemavu waliopo vijijini na kuwapatika huduma ya matibabu pamoja na vifaa mbalimbali.Hivyo aliwaomba wadau kujitokeza kusaidia ili Elimu juu ya kujikinga na mionzi ya jua kwa walemavu wa ngozi itolewe hadi vijijini ili kuiokoa jamii.

 ‘’’’’Tunashindwa kuwafikia wote kila wilaya na vijiji kutokana na kutokuwa na bajeti ya usafiri na nauli.Naiomba Serikali iguswe katika hili,pia ninawaomba wazazi kuwaleta watoto wao katika clinic  na waache kuwaficha ndani kwani mlemavu wa ngozi anatakiwa kupata huduma hii’’’’’Alisema Shing’oma


Kwa upande wake katibu wa chama cha watu wenye ulemavu wa Ngozi [TAS]Mkoa wa Iringa Leonansi Sambala alilishukuru shirika la USAID kwa kuwapatia vifaa vinavyosaidia watu wenye ulemavu wa ngozi kujikinga na mionzi ya jua ambayo inaweza letya athari kubwa kwao wakati wakifanya shughuli za maendeleo pamoja na wanafunzi.


‘’’’Mradi huu kutoka shirika la USAID ulipoanza ulilenga kumfikia kila mlemavu wa ngozi,pamoja na wafadhirikuleta mafuta tumeshindwa kuwafikia watu wenye ulemavu wa ngozi vijijini,hivyo tunaiomba serikali itusaidie na wadau watusaidie kusafirisha Albino walioko vijijini kuwaleta katika Hospitali ili waweze kupata huduma’’’’’’Alisema Sambala


Sambala aliwasihi Walimu kuwasaidia wananfunzi ambao ni walemavu wa ngozi kutowapa adhabu ya kukaa juani kwa muda mrefu,pia kuwapa kipaumbele kukaa mbele ya darasa kutokana na uono hafifu walionao ili waweze kusoma na kusikiliza kile kinachofundishwa.

‘’’’’Kwa mkoa wa Iringa walemavu wa Ngozi wapo 378 huduma haziwafii wote kutokana na swala la uwezashwaji kuwa ngumu,ikiwa nipamoja na baadhi ya wazazi kushindwa kuwaleta watoto wao katika Hospitali kwa ajili ya clinic’’’’’’alisema Sambala

0 maoni:

Chapisha Maoni