Maisha
ya kiungo wa Manchester City na timu ya taifa ya Ivory Coast, Yaya
Toure kwa pamoja na wachezaji walio na umri mkubwa ambao wanakipiga
pamoja Man City wanaweza kuwa na muda mchache wa kuendelea kuitumikia
klabu hiyo au kuondolewa haraka zaidi baada ya kutolewa kauli na
Mwenyekiti wa Man City, Khaldoon Al Mubarak ambayo inaonekana kuwa na
utata kuhusu wachezaji hao.
Akifanya
mahojiano na kituo cha CityTV, Mubarak alisema kuwa ni muda wa klabu
hiyo kuanza kuwapa nafasi vijana ili na wao waweze kuonyesha uwezo wao
na lakini pia kueleza kuwa kocha mpya wa klabu hiyo, Pep Guardiola
anataraji kufanya hivyo.
“Tunatakiwa kuweka ulingano wa umri, kati ya wachezaji wadogo na ambao wana uzoefu na haya yote yatafanyika kwa Pep,
“Pep
ana mfumo wake anavyotaka kuongoza kikosi lakini pia ana mfumo ambao
anataka utumike kucheza. Nahisi atahitaji wachezaji wa aina tofauti
tofauti ambao atawajumuisha katika kikosi chake,” alisema Mubarak.
0 maoni:
Chapisha Maoni