Picha na JOHN STEPHEN, Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).
…………………………………………………………………………………………………
Hospitali
ya Taifa Muhimbili (MNH) imepata viongozi wapya wa Chama cha
wafanyakazi wa Serikali na Afya Tanzania (TUGHE), Tawi la Muhimbili
katika uchaguzi uliofanyika leo majira ya alasiri katika ukumbi wa CPL
hospitalini hapo .
Nafasi
zilizogombaniwa ni pamoja na Mwenyekiti wa Tawi, Katibu wa Tawi,
wajumbe wa Halmashauri ya Tawi, nafasi ya Mwenyekiti Kamati ya wanawake,
Katibu kamati ya wanawake, Mjumbe kamati ya wanawake, Muweka Hazina
kamati ya wanawake, nafasi ya walemavu pamoja na nafasi ya vijana.
Katika
uchaguzi huo Bwana Mziwanda Salum Chimwege ametetea nafasi yake ya
Uenyekiti wa tawi na kuibuka kidedea kwa kupata kura 248, huku nafasi ya
Katibu ikichukuliwa na Bwana Faustine Fidelis Kaitaba ambaye amepata
kura 215.
Walioshinda
nafasi ya halmashauri ya tawi ni Idi Shaweja, Edina Maneno, Seif
Athuman, Rama Sultan, Yusuph Mkando, Adam Alfan, Josephine Lwambuka,
Shaban Zubery, Isaya Mbinga, Charles Kayombo, Aly Mkali, Musa
Mbuhita,Bure Nasoro, Joyce Chirwa, Mecktidis Chonga, Aikael Kisanga,
Hidal Mtoakani pamoja na Dk. Peter Kibacha.
Nafasi
ya Mwenyekiti kamati ya wanawake imechukuliwa na Zainab Mwagala kwa
kupata kura 71 huku Mwajuma Kisengo ameibuka mshindi kwa kupata nafasi
ya Ukatibu kwa kupata kura 75 .
Muweka
hazina kamati ya wanawake ni Halima Mayumana wakati nafasi ya vijana
imechukuliwa na Husein Jalala Mkangazi ambapo Salama Kasembe ameshinda
nafasi ya walemavu.
Awali
akifungua mkutano mkuu wa uchaguzi wa Tawi la TUGHE –Muhimbili , Kaimu
Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili-MNH- Profesa
Lawrence Museru ameupongeza uongozi uliopita wa TUGHE katika tawi hilo
kwa kushirikiana vema na Menejimenti pasipo migogoro.
Pamoja
na mambo mengine Profesa Museru amewaeleza wajumbe wa mkutano huo
kwamba kuanzia Julai mwaka huu MNH itaanza kutoa mkono wa heri kwa
wastaafu wake sanjari na kutoa posho kwa watumishi wote wa hospitali
hiyo.
“Posho
hizi zinatolewa si kwamba hospitali ina pesa nyingi lakini tunambua
mchango wa , kwani kila mmoja ametimiza wajibu wake hatua
iliyochangia kuongeza mapato ya hospitali , hivyo nawasihi sana
muendelee kufanya kazi kwa bidii ili suala hili liwe endelevu.”amesema
Profesa Museru.
Pia
ametumia fursa hiyo kuwasisitiza kwamba MNH itaendelea kuchua hatua
kwa wafanyakazi wasiio waaminifu katika utoaji wa huduma .
Viongozi hao wa TUGHE tawi la Hospitali ya Taifa Muhimbili wataongoza kwa muda wa miaka mitan






0 maoni:
Chapisha Maoni