Jumatatu, 6 Juni 2016

AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MAISHA KWA KOSA LA KUMLAWITI BINTI YAKE MWENYE UMRI MIAKA 7

MAHAKAMAya Hakimu Mkazi iringa imemhukumu Erick Philipo (35)mkazi wa kata ya Mkazi wilaya ya Iringa mkoani hapa kifungo cha maisha baada ya kukutwa  na hatia ya makosa matatu likiwamo la kumlawito mtoto wake wa kike wa  kumzaa  mwenye umri wa miaka  saba.
Akisomo hukumu hiyo jana Hakimu mkazi wa mahakama hiyo Andrew Scout alisema mahakama imeridhishwa na ushahidi uliotolewa na upande wa mashitaka mabao haujaacha shaka kuwa mtuhumiwa alitenda makosa hayo matatu kwa pamoja.
Makosa mengine katika kesi hiyo namba 72 ya mwaka 2015 ni pamoja na kuzini na ndugu yake kinyume na kifungu cha  227 sehemu ndogo ya ya tatu ya sheria ya ushahidi wa mtoto na kosa la tatu ni kumsababishia maaumivu mtoto huyo kinyume  kifungo hiocho hocho sehemu ndogo ya saba ya sheria ya ushahidi wa mtoto.
Scout alisema  kutokana na ushaidi uliotolewa mahakamani hapo, mtuhumiwa ametiwa hatiani kwa  makosa yote matatu na kwamba katika kosa la pili ambalo ni la kulawiti anahukumiwa kifungo cha maisha jela.
Adhabu nyingine katika kesi hiyo ni kosa la kwanza la kufanya tendo la ndoa na ndugu yake ambapo alihukumiwa kifungo cha miaka 30 jera na la tatu ni la kumsababishia maaumivu mlalamikaji ambapo alihukumiwa kifungo cha miaka mitano na kwamba adhabu hizo zitatkwenda pamoja.
“Katika kesi hii upande wa mashitaka ulioleta mashahidi nane na upande wa utetezi ulileta mashahidi 7,baad aya kusikiliza pande zote mbili upande wa mashitaka na jamuhuri,upande wa utetezi haujatoa ushahidi unaoweza kuishawishi mahakama kutomtia hatiani mtuhumiwa”alisema Scout.
Katika kesi hiyo upande wa jamuhuri uliongozwa na mwanasheria wa serikali Hope Charlesi aliyekuwa akisaidiwa na Happenes Flavian ambapo.
Wakili Charles aliitaka mahakama kumpa adhabu mtuhumiwa huyo kulingana na sheria zinavyotaka huku mtuhumiwa alipopewa nafasi ya kujitetea aliitaka mahakama kumpunguzia adhabu kwa mdai kuwa yeye anafamilia ya watu sita wanaomtegemea.
Katika hatua nyingine Mahakama hiyo ilimuhukumu kifungo cha miaka 30 jela Johnface  Lyang’oka baada ya kukutwa na hatia katika makosa mawili likiwamo la kukutwa na hatia ya kujihusisha na biashara ya Meno ya Tembo kinyume na sheria ya wanyamapori namba tano ya mwaka 2009.
Katika kesi hiyo alidaiwa kuwa mtuhumiwa huyo alikutwa na maneo 32 ya Tembo yenye thamani Sh 516 milioni na katika kosa la pili mtuhumiwa huyo alikutwa na vipande viwili vya pembe za ndovu vyenye thamani ya Sh 32.25 milioni.
Mtuhumiwa huyo pia ambaye  katika kesi hiyo namba …alishitakiwa alishitakiwa pamoja na mtuhumuiwa namba moja  Alfani Balo bani ambaye aliachiw ahuriwatuhumuwa
Kosa la pili mntuhumiwa huyo alikutwa na Vipande viwli vya pembe za ndovu kinyume na sheria vyethamani ya Sh 32 milioni kinyume na sheria ya uhujumu uchumi.
Katika shitaka hilo lililofunguliwa mahakani hapo Septemba 11 mwaka jana mtuhumiwa  huyo alishitakiwa pamoja na mtuhumiwa namba moja ambaye ni Alfani Balobani ambaye mahakama ilimuachia huru baada ya kutomkuta na hatia.
Mara baada ya kutolewa kwa hukumu hizo mbili Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesela ambaye alikuwa mahakamani hapo kusilikiza hukumu ya kesi ya ubakaji alielezea kufurahishwa kwake na hukumu hizo na kudai ni  mwanzo mzuri wa kampeni dhidi ya vitendo vya ubakaji na  unyangilki dhidi ya wanyama..
“Nimefurahishwa sana  hukumu za leo ,mahakama imetenda haki ,kumekuwa na kesi  nyinge za vitendo vya ubakaji na kupitia kesi hii mapambano dhidi ya watuhumiwa wa ubaakaji ndo yameanza”alisema Kasesela na kuongeza:
“Kuanzia sasa ninapiga marufuku mtu yoyote hususani wanandugu kumaliza kesi inayohusiana na vitendo vya ubakaji nyumbani na atakayebainiaka kufanya hivyo atachukulwiwa hatua kali za kisheria”alisema.

0 maoni:

Chapisha Maoni