Alhamisi, 2 Juni 2016

KWILAYA YA ILALA YAJIPANGA KUSAMBAZA MAENEO YOTE MAKASHA YA KUHIFADHIA TAKA

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi akizungumza wakati wa uzinduzi wa wiki ya mazingira duniani ambapo manispaa ya Ilala kwa kushirikiana na Kampuni ya usafi ya Green Waste Pro Ltd na nyingine kwa kufanya usafi katika fukwe za bahari ya Salender jana jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Sea-View Upanga, Victor Muneni na kulia ni Afisa Mazingira kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Ilala Bw. Abdon Mapunda.
 
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Sea-View Upanga, Victor Muneni akizungumza jambo na wadau wa mazingira waliokusanyika kwenye viwanja vya Salender Club kabla ya kuanza zoezi la usafi wa mazingira.
Baadhi ya wadau wa mazingira kutoka ofisi za Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, makapuni ya usafi yaliyopewa zabuni ya kusafisha manispaa ya Ilala ikiwemo Green Waste Pro Ltd, Vijana kutoka Roots and Shoot waliokusanyika kwenye uzinduzi wa wiki ya mazingira duniani iliyozinduliwa jana duniani kote.
Kiongozi wa dhehebu la Dawoodi Bohra nchini, Bw. Zainuddin Adamjee (wa pili kushoto) akimtambulisha Kiongozi Mkuu wa dhehebu la Dawoodi Bohra duniani, Ali Qadaar Syedi Mufadal bhaisaheb Saifuddin (wa tatu kushoto) kwa Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi (kulia) mara baada ya kuwasili jijini Dar es Salaam jana.
Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Joseph Sokoine (kushoto) akitoa salamu za serikali kwa Kiongozi Mkuu wa dhehebu la Bohora duniani, Ali Qadaar Syedi Mufadal bhaisaheb Saifuddin aliyewasili jana jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi akielezea mipango ya manispaa ya Ilala katika kuweka jiji safi wakati wa hafla fupi ya kukabidhiwa ‘Dustbin’ 53 zilizotolewa na Burhani Foundation Tanzania iliyofanyika katika mskiti wa dhehebu la Mabohra nchini.
Kiongozi Mkuu wa dhehebu la Dawoodi Bohra duniani, Ali Qadaar Syedi Mufadal bhaisaheb Saifuddin moja ya Dustbin kati ya 53 zilizotolewa na Burhan Foundation kwa Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi katika hafla fupi iliyofanyika nyumbani kwa Kiongozi huyo jijini Dar es Salaam.

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi akimshukuru Kiongozi Mkuu wa dhehebu la Dawoodi Bohra duniani, Ali Qadaar Syedi Mufadal bhaisaheb Saifuddin kwa zawadi ya kikoi.
Afisa Mazingira kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Ilala Bw. Abdon Mapunda akipokea zawadi ya kikoi kutoka kwa Kiongozi Mkuu wa dhehebu la Dawoodi Bohra duniani, Ali Qadaar Syedi Mufadal bhaisaheb Saifuddin.

0 maoni:

Chapisha Maoni